• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri apongeza Mpango na Bajeti ya Jiji Dodoma

Imewekwa tarehe: February 11th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imepongezwa kwa kuandaa vizuri Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023 kwa kuzingatia miongozo na vipaumbele vilivyowekwa ikitajwa kuwa itakwenda kujibu changamoto katika jamii.

Pongezi hizo zilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akiongea katika kikao maalum cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Dodoma cha kupitia mapitio ya bajeti ya mwaka 2021/ 2022 pamoja na mpango wa makisio ya mapato na matumizi ya mwaka 2022/2023 kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashauiri hiyo leo.  

Shekimweri alipongeza miongozo mbalimbali na vipaumbele vilivyowekwa na Jiji la Dodoma katika Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2022/2023. Aidha, alipongeza andiko la Mpango na Bajeti ya halmashauri chini ya Mkurugenzi na timu yake ya menejimenti na kulitaja kuwa ni andiko zuri linalojitosheleza kujibu changamoto za wananchi wa Jiji la Dodoma.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amekuwa akitoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo kwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na kuongeza kuwa fedha zote zinafika kwa wakati. Alisema kuwa Jiji la Dodoma limekuwa kilifanya vizuri katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Alisema kwa fedha shilingi bilioni 2.940 zilizotolewa katika fedha za mapambano dhidi ya UVIKO-19, madarasa yote 147 pamoja na samani zake yamekamilika. Alisisitiza kuwa changamoto iliyopo ni ya uwiano wa madarasa, wanafunzi na matundu ya vyoo, na kushauri bajeti hiyo iongeze ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule katika jiji hilo.

Aidha, alishauri halmashauri ianze kuainisha maeneo yenye uhitaji wa madarasa mengine na kujipanga kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya ghorofa. Alisema kuwa sababu kubwa ni maeneo yaliyopo ni yaleyale hayaongezeki.

Akiongelea Mpango na Bajeti wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2022/2023 Mchumi wa Jiji la Dodoma, Francis Kaunda alisema kuwa Mpango na Bajeti umezingatia vipaumbele mbalimbali. Alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka wa fedha 2022/2023 imejipanga kuelekeza nguvu zake katika kuweka mazingira wezeshi yatakayosababisha kuinua na kukuza uchumi wa halmashauri na kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja kwa kuwekeza katika miundombinu ya uchumi na kutoa mikopo kwa wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. “Fedha zitakazotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, asilimia 60 ya kiasi hicho kitaelekezwa kwenye miradi yenye tija itakayozalisha ajira. Kufungua akaunti kwa ajili ya marejesho ya asilimia 10 ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Pia marejesho hayo ya mikopo ya asilimia 10 yanayotarajiwa kurejeshwa na vikundi vilivyokopeshwa yataingizwa kwenye Mpango na Bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023” alisema Kaunda.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.