• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri aridhishwa ujenzi barabara Mji wa Serikali

Imewekwa tarehe: September 9th, 2021

Na Sifa Stanley na Binde Constantine, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameridhishwa na maendeleo ya ujenzi wa barabara katika Mji wa Serikali Mtumba zinazojengwa na Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Dodoma.

Mkuu huyo wa Wilaya alifanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara unaoendelea katika mji wa serikali na kusimamiwa na TARURA Wilaya ya Dodoma.

Shekimweri alisema kuwa ameridhishwa na ujenzi wa barabara unaoendelea katika mji wa serikali. Aliagiza kukamilisha mradi huo ifikapo tarehe 31 Disemba, 2021 kwa mujibu wa makubaliano ya mkataba ili barabara hizo zianze kutumika. “Mmetoa sababu za kuchelewesha mradi, tumewaongeza miezi mitano. Miezi mitano ni mingi, simamieni mradi ili ukamilike kwa muda uliopangwa” alisema Shekimweri.

Aidha, aliagiza suala la upandaji miti katika barabara hizo ili kuendelea kutunza mazingira. Alisema kuwa upandaji miti ni utekelezaji wa ajenda ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kupanda miti na kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.  “Tutekeleze ajenda ya Makamu wa Rais ya kupanda miti kwa kuhakikisha tunapanda miti, mradi unapoendelea wadau wakijitokeza hasa wa mazingira tuwape nafasi ya kupanda miti” aliongeza Shekimweri.

Naye Mkurugenzi wa Barabara za Mijini kutoka TARURA, Mhandisi Mohamed Mkwata akizungumzia maendeleo ya mradi huo, alimhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa mradi utakamilika kwa wakati. Alisema kuwa Mkandarasi ameongeza juhudi katika utekelezaji wa mradi ili ukamilike kwa wakati. “Mkandarasi ameongeza mitambo na vifaa vya ujenzi ikiwemo mitambo ya kusaga kokoto na mitambo ya kuzalisha lami. Pia anafanya kazi siku zote za wiki ili kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati” alisema Mhandisi Mkwata.

Mkuu wa Wilaya alifanya ziara katika maeneo makuu mawili ya mradi huo ambayo ni eneo la kusini na eneo la kaskazini, eneo la kusini la mradi huo limetengwa mahususi kwa ujenzi wa ofisi za wizara za Serikali na mabalozi, eneo la kaskazini limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za ubalozi wa Marekani na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.