• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri aridhishwa ujenzi sekondari Hombolo Makulu

Imewekwa tarehe: May 27th, 2022

Na. Theresia Francis, DODOMA

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri  ameridhishwa na kupongeza hatua ya ujenzi wa mradi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu unaoendelea kujengwa katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa gharama ya shilingi milioni 470.

Alitoa pongezi hizo katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Wilaya ya Dodoma, alipotembelea ujenzi wa sekondari hiyo katika Kata ya Hombolo Makulu jijini hapa jana.

Mkuu huyo wa wilaya baada ya kutembelea na kukagua ujenzi wa shule hiyo, alisema kuwa ameridhishwa na hatua ya ujenzi unaoendelea. Alisema kuwa mradi huo una akisi fedha iliyotolewa na serikali kuu chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Shekimweri alishtushwa kuona ndani ya mradi huo kuna nyumba binafsi imejengwa na kusema kuwa kitendo hicho kinahatarisha usalama wa wanafunzi na wafanyakazi katika mradi huo. Alimuagiza Kamanda wa Polisi wa Wilaya kumchukulia hatua mmiliki wa nyumba hiyo. "Nilitoa maelekezo mara ya mwisho kuhusu nyumba ile iliyopo ndani ya mradi wa shule naona hamkulifanyia kazi. Sasa OCD mchukulie hatua mmiliki wa nyumba hiyo" alisema Shekimweri kwa ukali.

Kwa upande wake Afisa elimu ya sekondari wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alitoa shukrani kwa Serikali kwa kufanikisha ujenzi wa mradi huo wa shule ya sekondari. Alisema kuwa shule hiyo ina jumla ya madarasa nane, Maabara tatu, jengo la Maktaba, jengo la TEHAMA pamoja na matundu 20 ya vyoo.

“Shule hii ni mkombozi katika kata yetu, wanafunzi wamekua wakitembea umbali mrefu zaidi ya kilomita tisa kufuata huduma ya elimu. Hivyo, basi shule hii itasaidia kwa kiasi kikubwa watoto wetu hususani watoto wa kike" alisema Mwalimu Rweyemamu.

 Katika ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma aliambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya, Afisa elimu ya sekondari wa Jiji la Dodoma, Diwani wa Kata ya Hombolo Makulu pamoja na maafisa waandamizi wa serikali.


Mheshimiwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri (wa tatu kutoka kulia) alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Hombolo Makulu akiambatana na Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari wa Jiji la Dodoma Mwalimu Upendo Rweyemamu.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.