• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri ataka Jiji safi

Imewekwa tarehe: August 27th, 2021

Na Sifa Stanley, Dodoma

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameiagiza Halmashauri ya Jiji na wadau mbalimbali wa utunzaji wa mazingira Jijini Dodoma kuhakikisha mazingira ya Jiji hilo yanafanyiwa usafi, na kuwa safi muda wote na kutunzwa.

Shekimweri alisema hayo wakati wa kikao kazi cha wadau wa mazingira kilichofanyika katika ukumbi wa Polisi jamii Agosti 26, 2021 kwa lengo la kubadilishana uzoefu na kuainisha changamoto mbalimbali za kimazingira Jijini humo.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa ni wajibu wa viongozi kusimamia suala la usafi wa mazingira, pia wadau wa mazingira lazima wawajibike katika utunzaji wa mazingira ili kuliweka Jiji la Dodoma katika hali ya usafi.

“Sisi ni jiji la sita, sisi ni Makao Makuu, tumejengewa soko kuu kubwa, uwanja mzuri wa ndege unajengwa, na stendi nzuri, kwa uwekezaji huu wote tuliofanyiwa na Serikali hivi kweli tuchafue mazingira?, tuhakikishe tunatunza mazingira ili iwe kama njia ya kuishukuru Serikali ya awamu ya tano na sita kwa maendeleo waliyotufanyia”alisema Shekimweri.

Naye Mkuu Wa Idara ya Mazingira na Udhiti Taka Ngumu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alieleza namna idara hiyo inavyofanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha mazingira ya Jiji yanatunzwa, na usafi katika Jiji unaimarika ikiwemo suala la kufanya usafi kila Jumamosi ili kuhakikisha jiji linaendelea kuwa safi wakati wote.

“Tunaendelea kuhimiza utunzaji wa mazingira, na zoezi la usafi kila jumamosi ni endelevu ambapo Jumamosi hii tutakuwepo Kata ya Kilimani kwa ajili ya kuungana na wakazi wa Kata hiyo kuhamasisha na kufanya usafi pamoja” alisema Kimaro.

Akisisitiza suala la kutunza mazingira, Afisa Mazingira na Udhibiti Taka Ngumu katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Ally Mfinanga aliwataka wadau hao wa mazingira kutumia njia sahihi za utunzaji taka na kuepuka uchomaji na ufukiaji wa taka ili kuepusha uchafuzi wa mazingira huku akiwakumbusha kuendeleza tabia ya upandaji miti ili kuendelea kuweka mazingira katika hali ya usafi na usalama.

“Kwa wakazi wote wa Tarafa ya Dodoma Mjini, ni marufuku kuchimba mashimo ya taka na kuchoma taka, vitendo hivyo vinachangia kuchafua mazingira” alisema Mfinanga.

Wadau wa mazingira walioshiriki kikao kazi hicho ni pamoja na Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA), Wakala wa Barabara za Mjini na Vijijini Tanzania (TARURA), Wakala wa Barabara (TANROADS), Makampuni yanayojishughulisha na kazi za usafi, wadau wa erejelezaji wa taka, na watendaji mbalimbali wa ngazi ya Kata.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.