• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri atoa maagizo makampuni ya usafi

Imewekwa tarehe: January 29th, 2022

MKUU wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri ameyataka makampuni yaliyopata kandarasi ya usafi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma kufanya kazi hiyo kwa kiwango na kuhakikisha jiji linakuwa safi ili kuwaepusha wananchi dhidi ya magonjwa mbalimbali.

Agizo hilo alilitoa wakati akiongea na wamiliki wa makapuni ya usafi waliopata kandarasi ya kufanya usafi katika Jiji la Dodoma na wananchi waliojitoleza katika zoezi la usafi lililofanyika katika kata ya Kikuyu Kaskazini leo.

Shekimweri alisema “nawapongeza kwa kupewa kandarasi hii, lakini nawapa pole kwa sababu kwa kweli tutakuwa wakali sana kwenye changamoto tunayokuta kwenye maeneo mengi ya kuzagaa kwa taka. Wananchi hawa rahimu wana muitikio kama huu watafanya usafi na kupeleka kwenye ‘collection point’ na nyie mchukue hamuendi kuchukua. Katika hili tutagombana sana. Mkurugenzi nimefurahi umewapatia mkataba wa mwaka mmoja makusudi ili tuwapime. Nataka Mkurugenzi usimamie mkataba ule vizuri”.

Akijibu swali kuhusu maeneo ya viwanja ambavyo havijaendelezwa na kugeuzwa kuwa maeneo ya kutupwa takataka, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema kuwa maeneo hayo yatafutwa. “kuhusu mapagale na vichochoro, nitatuma timu ya wataalam Jumatatu itembelee mitaa yote kuanza na Kikuyu. Tuangalie viwanja gani vipo wazi, viwanja gani vinamapale ambayo hayajakamilika na vichochoro. Kwa wenye viwanja ambavyo hawajaendeleza walipewa miezi 36 kuwa wameviendeleza. Tutaorodhesha viwanja hivyo na kupeleka kwenye kamati ya ugawaji wa Ardhi na kupeleka kwa Kamishna vifutwe kwa ajili ya watu wenye nia ya kuendeleza” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu, Dickson Kimaro alisema kuwa suala la usafi ni ustaarabu. Aidha, aliyataja makampuni yaliyopata kandarasi ya usafi kuwa ni Al Jabry Investment iliyopewa kata ya Uhuru na Kiwanja cha Ndege. JKT Suma Cleaning and Fumigation imepewa Kata ya Viwandani, Makole, Tambukareli, Madukani. Kampuni ya tatu aliitaja kuwa ni Wejisa Company Ltd iliyopewa Kata ya Majengo na Kilimani.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.