• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

DC Shekimweri “Badilisheni Changamoto na kuzifanya fursa zenye mafanikio kwa jamii”

Imewekwa tarehe: September 3rd, 2024

Na. Jackline Patrick na John Masanja, DODOMA

MASHIRIKA yasiyo ya Kiserikali yametakiwa kuzitazama changamoto mbalimbali katika jamii na kuzitumia kama fursa kwa utoaji wa elimu na kuisaidia jamii kuondokana nazo.

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri alipokuwa akizungumza na wadau mbalimbali walioshiriki katika Jukwaa la Mwaka la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Dodoma. Jukwa hilo limefanyika Agosti 27,2024 katika ukumbi wa mikutano, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa (Mkapa House).

Akizungumza wakati wa hotuba yake,Mhe. Shekimweri aliyapongeza Mashirika yasiyo ya Kiserikali katika jitihada zake za kuihudumia jamii kwenye masuala mbalimbali ya kimaisha kupitia huduma wanazozitoa, huku akiwataka kuzidi kuisaidia Serikali.

Aidha, Mhe. Shekimweri aliyataka Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kuisaidia Serikali katika kutoa elimu itakayozuia ukatili kwa watoto, unyanyasaji wa kijinsia pamoja matumizi ya dawa za kulevya. Alisema masuala hayo yamekuwa ni changamoto kubwa katika jamii ya sasa.

“Mashirika Yasiyo ya Kiserikali yafanye kazi kwa uhuru, kwa kuzingatia sheria, kanuni. Kazi ifanyike kwa uzalendo kwa kuzingatia maadili ya Nchi yetu” alisisitiza  Shekimweri.

Sambamba na hayo,Shekimweri  aliwapongeza wajumbe kwa kuhudhuria katika Jukwaa hilo, na kuwataka kwenda kuyafanyia kazi yote waliyojifunza kwa ustawi na maendeleo ya jamii.

Awali wakati wa ufunguzi, Msajili Msaidizi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Dodoma, Honoratha Rwegasira alisema lengo kuu la jukwaa hilo ni kuimarisha mahusiano baina ya Serikali, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Wadau wengine pamoja na kutambua mchango wa mashirika hayo katika maendeleo ya Nchi.

"Kuna malengo mahususi ambayo ni kuimarisha mahusiano ya Serikali na wadau wengine kwa ajili ya kutambua mchango wa Mashirika Yasio ya Kiserikali ambapo tumekusudia katika Jukwaa hili kujadili namna mashirika haya yanavyoshiriki kutekeleza mipango ya kitaifa".Alisema Rwegasira.

Vilevile aliongezea kwa kusema “Wadau wote waweze kushirikiana, kuleta huduma bora, kuimarisha uchumi ili kumhudumia Mwanachi, kujenga uelewa wa pamoja kuhusu uratibu na usimamizi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, maana kuna mashirika ambayo ni machanga, hivyo watakapokutana na wazoefu wataweza kupata uwelewa mkubwa na kushirikishana katika fursa, changamoto na mafanikio".

Rwegasira alihitimisha kwa kusema kuwa jukwaa hilo ni fursa mojawapo, kwasababu wajumbe wataweza kubadilishana mawazo na kujenga urafiki wa pamoja kwa ajili ya maendeleo na uhusiano mzuri.

 Kaulimbiu ya Jukwaa la Mwaka la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Dodoma 2024 ni “Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ni Wadau Muhimu, Washirikishwe Kuimarisha Utawala Bora".





Matangazo

  • TANGAZO LA MABADILIKO YA TAREHE YA USAHILI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA WASIMAMIZI JIMBO LA MTUMBA October 03, 2025
  • MAJINA YA WASIMAMIZI WA VITUO VYA KUPIGIA KURA- DODOMA MJINI October 03, 2025
  • TANGAZO LA MAJINA YA MAKARANI WAOGOZAJI WAPIGA KURA October 03, 2025
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Rc Senyamule awasihi wawekezaji sekta binafsi kuwekeza Dodoma

    October 03, 2025
  • CCTV kamera mwarobaini wa wavunjifu wa sheria jiji la Dodoma

    October 02, 2025
  • Wadau wa afya wapongezwa kwa juhudi zakudhibiti vifo vya wajawazito

    October 01, 2025
  • UONGOZI WA KLABU YA MICHEZO OFISI YA MKUU WA MKOA WA DODOMA WAKUTANA NA RAS KAZUNGU

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.