• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Ma-DC Dodoma kusimamia katazo mifuko ya Plastiki

Imewekwa tarehe: June 1st, 2019

Wakuu wa wilaya mkoani Dodoma wametakiwa kusimamia katazo la serikali la matumizi ya mifuko ya plastiki katika maeneo yao ikiwa ni utekelezaji wa sheria ya nchi.

Kauli hiyo imetolewa na mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Patrobas Katambi katika uzinduzi wa kikosi kazi cha ukaguzi wa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki tukio ambalo limefanyika katika eneo la ‘Independent square’ jijini Dodoma leo.

Wakazi wa Jiji la Dodoma walioshiriki uzinduzi wa kikosi kazi cha kusimamia katazo la mifuko ya plastiki wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini Mhe. Patrobas Katambi

Katambi amesema “Dodoma lazima tuwe wa mfano, tusirudi nyuma, tusiwaangushe viongozi wetu. Leo natangaza rasmi kuwa waheshimiwa wakuu wa wilaya wote wa Mkoa wa Dodoma wasimamie katazo la Serikali la matumizi ya mifuko ya plastiki”. Halmashauri ya Jiji la Dodoma, inatakiwa kuwa jiji la mfano katika kumpa heshima Rais Dkt John Magufuli, aliongeza. Aidha, alisema kuwa halmashauri ya jiji la Dodoma itakuwa ya kwanza katika usafi wa mazingira kitaifa mwaka 2019.

Mkuu huyo wa wilaya aliwataka wananchi kutafuta na kupata uelewa wa taarifa mbalimbali zinazohusu makatazo ya mifuko hiyo ili kuepuka adhabu zilizowekwa. Alionya kuwa, mtu kutojua sheria si kigezo cha kumfanya asiadhibiwe pale ambapo atapatikana na kosa la kuvunja sheria. “Wajibu wa wananchi ni kutafuta taarifa sahihi za makatazo ya mifuko ya lastiki. Zoezi la ukaguzi linapoanza atakayekutwa na mifuko ya plastiki atapigwa faini kwa mujibu wa sheria” alisema Katambi.

Akiongelea kikosi kazi cha ukaguzi, Katambi amesema “Nazindua rasmi kikosi kazi kitakachoenda kukagua mifuko la plastini katika maeneo mbalimbali. Kikosi kazi hiki tupo vizuri, usithubutu kukaidi katazo hili. Akifafanua zaidi Katambi  amesema faida kubwa ipo kwetu wananchi tunapoacha matumizi ya mifuko ya plastiki, hivyo ni vizuri mkaamini kuwa viongozi wetu wana maono ya mbali kwa nchi yetu” alisema Katambi.

Viongozi wakishiriki katika kufanya usafi katika mtaa wa 'One way' jiji Dodoma kabla ya uzinduzi rasmi wa kikosi kazi ya katazo la mifuko ya plastiki.

Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Maduka Kessy alisema “leo tunazindua rasmi katazo la mifuko ya plastiki. Ni vizuri wote kuelewa kuwa hili ni zoezi za kudumu, si la mpito”. Aidha, aliongeza kuwa wasafiri wanaopita Dodoma watakaguliwa ili kuwabaini watakaokuwa na mifuko hiyo. Hakutakuwa na masuala ya kisiasa katika utekelezaji wa katazo hilo, aliongeza.

Awali mkuu wa idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu wa Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro aliwapongeza wananchi wote waliojitoleza kushiriki katika zoezi la kuzibua mifereji na kuondoa mifuko la plastiki iliyokuwa ikisababisha mifereji hiyo kuziba.

Nae mfanya biashara katika eneo la barabara ya "One way", Shio Patrick alipongeza zoezi la usafi lililofanyika katika eneo hilo na kushauri liwe endelevu. “Changamoto kubwa ya usafi katika eneo hilo ni baadhi ya wenye nyumba kukaidi kutoka kufanya usafi. Naomba serikali iwahamasishe wenye nyumba hao kutoka na kushiriki pamoja na watu wengine kufanya usafi” alisema Patrick.

Wakazi wa Jiji la Dodoma, watumishi wa Jiji na wafanyakazi wa Kampuni ya usafi ya Green Waste wakifanya usafi kwenye mfereji wa 'Pombe River'

Uzinduzi wa kikosi kazi kwa ajili ya ukaguzi wa katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki ulitanguliwa na zoezi la usafi lililofanyika barabara ya nane na ‘One way’ likiongozwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma Maduka Kessy.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.