• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Deni la Taifa lafikia Trilioni 54/-

Imewekwa tarehe: January 2nd, 2020

DENI la serikali ni himilivu, japokuwa hadi Novemba 30, 2019 limefikia Sh trilioni 54.84 sawa na ongezeko la asilimia 11.7 ikilinganishwa na Sh trilioni 49.08, Novemba 2018, imeelezwa.

Akizungumza jijini hapa, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alisema kati ya kiasi hicho, deni la nje ni Sh trilioni 40.39 na deni la ndani ni Sh trilioni 14.44.

Waziri Mpango alisema ongezeko la deni hilo, limetokana na riba ya mikopo, ambayo mikataba yake iliingiwa zamani na mikopo mipya yenye masharti nafuu na ya kibiashara kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Mpango alisema mikopo hiyo imetumika kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo, ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli na viwanja vya ndege, ujenzi wa mitambo ya kufua umeme na utekelezaji wa miradi ya maji.

Alisema tathmini ya uhimilivu wa deni iliyofanyika Desemba 2018, inaonesha kuwa deni ni himilivu kwa muda mfupi, wa kati na mrefu, kwa kuzingatia vigezo muhimu vinavyotumika kimataifa.

Vigezo hivyo ni uwiano wa deni la serikali kwa Pato la Taifa ni asilimia 27.2 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 70.

“Uwiano wa deni la nje pekee kwa Pato la Taifa ni asilimia 22.2 wakati ukomo ni asilimia 55,” alisema.

Alisema uwiano wa deni la nje kwa mauzo ya nje ni asilimia 157.3 wakati ukomo ni asilimia 240. Dk Mpango alisema ulipaji wa deni la nje, kwa kutumia mauzo ya bidhaa nje ni asilimia 15.2 ikilinganishwa na ukomo wa asilimia 23.

Alisema hiyo ina maana kuwa Tanzania bado ina uwezo wa kuendelea kukopa kutoka ndani na nje ya nchi ili kugharamia shughuli zake za maendeleo na kulipa mikopo, inayoiva kwa kutumia mapato yake ya ndani na nje kwa wakati.

Dkt. Mpango alisema Desemba 2019, serikali pia imefanya tathmini hiyo na matokeo ya awali hayatofautiani na tathmini ya Desemba 2018. Matokeo rasmi ya tathmini mpya, yatatolewa baada ya uchambuzi unaendelea kukamilika.

Chanzo: habarileo.co.tz



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.