• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Diwani 'awafunda' wahitimu chuo cha DOMECO

Imewekwa tarehe: December 27th, 2019

DIWANI wa Kata ya Majengo, Mhe. Msinta Mayaoyao amewataka  wahitimu wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Dodoma kuzingatia umakini na weledi katika kazi zao kutokana na umuhimu wa taaluma yao katika maendeleo ya nchi na ulimwengu kwa ujumla.

Aliyasema hayo mwishoni mwa wiki kwenye Mahafali ya chuo hicho yaliyofanyika jijini Dodoma, katika hotuba yake aliwasisitiza wahitimu hao kuzingatia ukweli na usahihi wa maudhui wanayoyawasilisha kwenye mitandao ya kijamii na hata wawapo katika utekelezaji wao wa majukumu ya kazi. Alisema kuwa kufanya hivyo kutawajengea kuaminika na kuheshimika katika jamii.

Mhe. Mayaoyao alisema hayo kutokana na ongezeko kubwa la waandishi wanaosambaza taarifa ambazo hazijafanyiwa uchunguzi wa kitaaluma juu ya ukweli wa habari hizo. Kufanya hivyo kunapelekea jamii kutokuwa na imani na waandishi wa habari na taaluma ya habari kwa ujumla wake.

“Taaluma ya habari ni nyeti, na ni muhimu sana duniani. Tumieni elimu mliyoipata hapa ipasavyo, mkaoneshe utofauti kati ya ninyi wasomi na wale makanjanja wanaofanya kazi ili mkono uende kinywani. Endelezeni na mkawe mfano kama ilivyo kwa wakongwe wa tasnia hii”.

“Lakini  kamwe hamuwezi kuwa waandishi wazuri kama mtakuwa hamjui kuutafuta ukweli wa jambo, kwani mnaweza kusababisha matatizo makubwa na hata kuwa chanzo cha migogoro miongoni mwa watu katika jamii,” alisema Mhe. Mayaoyao.

Mbali na hayo Diwani huyo alisisitiza juu ya kujenga uaminifu miongoni mwa jamii na ushirikiano, ili kurahisisha na  kuwajenga wahitimu hao katika kuendea maisha ya mitaani hasa katika upande wa soko la ajira.

“Ushirikiano ni nguzo ya mafanikio, kokote muendako  kumbukeni hili. Fanyeni kazi kwa kuzingatia miiko ya taaluma yenu, nidhamu pia itawabeba heshimianeni haijalishi ni mkubwa au mdogo. Simamieni misingi ya ukweli wa taarifa mkaonyeshe utofauti katika tasnia hii ya habari,” alisema Diwani huyo.

Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Dodoma kilifanya mahafali yake ikiwa ni kwa mara ya pili, awamu ya kwanza kuyafanyia jijini hapa huku ya awamu iliyopita ikifanyika mkoani Morogoro.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.