• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt Biteko afungua rasmi maonesho ya wiki ya Nishati, 2024

Imewekwa tarehe: April 15th, 2024

NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amefungua rasmi maonesho ya Wiki ya Nishati katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma ambapo amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha  Sekta ya Nishati  kutokana na nyenzo na maelekezo anayoyatoa ambayo yamempambanua kama kiongozi anayetatua matatizo ya wananchi kwa kutenda zaidi na sio maneno.

Dkt. Biteko amesema maelekezo  ya Rais, Dkt. Samia pamoja na nyenzo anazozitoa kwa Wizara ya Nishati zimepelekea nchi sasa kuwa na umeme wa kutosha na kwamba  hakuna mgawo tena huku kukiwa na mitambo ambayo ipo standby kuwashwa pale inapotokea hitilafu kwenye mitambo mingine ya uzalishaji umeme.

Aidha, kwa mikoa ambayo ipo nje ya gridi ya Taifa ikiwemo Katavi, Rukwa, Kigoma, Lindi na Mtwara, amesema kuwa yote itaunganishwa kwenye gridi ya Taifa kwani Rais, Dkt. Samia ameshatoa fedha za kutekeleza miradi ya umeme itakayoiunganisha mikoa hiyo na gridi ambayo tayari inaendelea.


Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ameipongeza TANESCO kwa kuendelea kuimarisha utendaji kazi wao ikiwemo utatuzi wa changamoto za umeme akitolea mfano athari iliyotokea katika gridi ya umeme usiku wa siku ya Pasaka kutokana na hitilafu kwenye mfumo wa kudhibiti kiwango cha  maji kwenye mitambo ya Kidatu ambapo tatizo hilo lilipaswa kushughulikiwa kwa siku tatu lakini TANESCO ilifanya jitihada na kutatua changamoto hiyo kwa muda wa masaa kadhaa.

Pamoja na pongezi  hizo Dkt. Biteko ametoa angalizo kwa kampuni tanzu za TANESCO  kuhusu utendaji kazi wao ikiwemo Kampuni ya Uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania (TGDC) ambapo kampuni hiyo ilitoa ahadi ya kuanza uchorongaji wa visima vya Jotoardhi katika eneo la Ngozi Mbeya tarehe 1 Aprili 2024 lakini bado hawajaanza kazi hiyo  hivyo amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati kuisimamia ipasavyo kampuni hiyo ili nchi iweze kupata umeme wa Jeothemo.

Pamoja na uendelezaji wa Sekta ya Umeme, Dkt. Biteko amesema kuwa Wizara inaendelea na utekelezaji wa mipango mingine ikiwemo wa nishati safi ya kupikia ambapo Baraza la Mawaziri limeshapitisha Mpango Mkakati wa Nishati safi ya kupikia na sasa kinachofanyika ni utekelezaji

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.