• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt Gwajima aikaribisha MEWATA kushirikiana na Wizara

Imewekwa tarehe: April 24th, 2024

Na WMJJWM, Dar Es Salaam

SERIKALI imetoa wito kwa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania, MEWATA kufanya kazi kwa pamoja kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum ili kutatua changamoto mbalimbali ndani ya Jamii zenye matokeo hasi kwenye afya.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima, alipokuwa akifungua Mkutano wa 21 wa Mwaka wa chama hicho, Aprili 21, 2024 jijini Dar Es Salaam.

Waziri Dkt. Gwajima amebainisha kuwa, changamoto nyingi kwenye jamii hupelekea matokeo yenye athari za kiafya mathalani msongo wa mawazo, afya duni ya akili na hata ukatili wa kijinsia unaodhuru afya, ambapo msingi mkubwa ni jamii kutoelewa jinsi gani baadhi ya mitindo ya maisha, mila, tamaduni na desturi zao zina athari kubwa kwenye afya kuanzia umri wa awali wa mtoto, ujana hadi uzee.

“MEWATA kama taasisi ya madaktari wanawake ina nafasi ya kufanya mapinduzi makubwa kwenye jamii kwa kupeleka elimu na huduma. Mambo mengi tunayoyaona huku juu kama changamoto ikiwemo ukatili wa kijinsia, ndoa kuvunjika, watoto wa mitaani, mila kandamizi yanaweza kudhibitiwa iwapo MEWATA itaingia kwenye kutoa elimu ndani ya jamii na kutokomeza mizizi ya changamoto hizi”. Amesema Dkt. Gwajima.

Aidha, ameiomba MEWATA kutumia taaluma zao kikamilifu bila aibu pale wanapohudumia wagonjwa, kuchambua hali ya ugonjwa na historia za maisha ya kijamii ili kubaini msingi wa tatizo la afya kutokana na maisha ya kijamii.

Kwa upande wake rais wa Chama hicho Dkt. Zaitun Bohari amesema kuna changamoto nyingi wanazopata wanawake ambazo hazizungumzwi kwenye jamii kutokana na mila na desturi kandamizi, hivyo kwa MEWATA ni changamoto mojawapo ya kufanyia kazi kuhakikisha inatoa elimu ya afya kwa wanawake hasa vijijini.

Baadhi ya wanachama wa MEWATA walioshiriki mkutano huo kutoka maeneo mbalimbali nchini, wameishukuru Serikali kwa ushirikiano na kuahidi kuendelea kutoa mchango kama chama cha kitaaluma kwa kuboresha afya ya mama na mtoto kwa ustawi wa jamii nzima.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.