• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt. Mahenge apambania Dodoma iwe karibu na Hifadhi

Imewekwa tarehe: October 15th, 2020

SHILINGI bilioni 2.8 zinahitajika kwa ajili ya kufungua barabara kati ya Dodoma na Mbuga ya Wanyama ya Ruaha ili kuvutia watalii kutoka mkoani humo kwenda kuona vivutio katika hifadhi hiyo.

Meneja wa Tarura Wilaya ya Chamwino, Nelson Maganga alisema fedha hizo zikipatikana barabara hiyo itaboreshwa na kuwa katika kiwango bora cha kupitika wakati wote wa mwaka.

Maganga alisema, fedha hizo zikipatikana zitafungua barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 121 hadi Hifadhi ya Ruaha na hivyo kupunguza safari ya watalii kuzunguka Iringa kwenda umbali wa kilometa 368 kufika hifadhini.

Maganga alisema, barabara hiyo yenye kipande cha kilometa 30 za lami hadi Mpunguzi, itahitajika fedha za kurekebisha kipande cha kilometa 91 ili iwe katika kiwango bora cha kupitika msimu wote.

Tarura tayari wanaendelea na marekebisho kutokana na bajeti waliyopata mwaka jana 2018/19 ya Sh milioni 181 na ya mwaka huu 2019/20 ya sh milioni 171 katika kipande cha Manda hadi Mpunguzi.

Lakini kama fedha zingepatikana ingewezekana kuboresha kipande cha Manga hadi Ilangali kilometa 25 hadi kuwenda mpaka wa Dodoma na Iringa ili kuingia kwenye hifadhi hiyo.

Alisema juhudi za kufungua barabara hiyo zinafanyika kupitia Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge ambaye pamoja na wadau wengine amepita barabara hiyo na kushuhudia kwamba ni fupi sana kufika hifadhini.

Alisema Dkt. Mahenge anaendelea na mzungumzo na wizara ya maliasili na utalii ili kuona ni namna gani wanaweza kuunga mkono juhudi za mkoa kutaka kuifungua barabara hiyo ambayo ni muhimu katika kupeleka watalii kutoka Dodoma.

Alisema kabla ya kuingia kwenye hifadhi itatakiwa kujengwa karavati ambalo litarahisisha kuvuka na kuingia kuona wanyama katika hifadhi hiyo kupitia mkoani Dodoma.

Mkakati wa Mkuu wa Mkoa ni kualika wadau mbalimbali ikiwemo Wizara ya Maliasili na Utalii, taasisi ya TAWA, TANAPA, TAWIRI na taasisi nyingine kwa lengo kutembelea hifadhi kupitia njia hiyo ili kupiga picha na kutengeneza makala ambayo itauzwa kwa lengo la kupata fedha za kuboresha barabara na miundombinu mengine ili kufika hifadhini kwa njia hiyo fupi.

Barabara ya Dodoma - Mbuga ya Wanyama ya Ruaha ikiboreshwa itasaidia kuwapa fursa watalii wanaofika jijini Dodoma kupitia Uwanja wa Ndege wa Msalato, Reli ya Kisasa (SGR) na kupitia njia nyingine, hivyo watapata fursa ya kutembelea hifadhi hiyo yenye sifa ya kuwa na wanyama wengi kupitia Dodoma kuliko kuzunguka Iringa.

Chanzo: HabariLeo


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.