• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt. Mahenge aridhishwa na utendaji kazi Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: June 9th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge ameridhishwa na utendaji kazi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma hadi kupata hati safi katika ukaguzi wa hesabu za serikali za mwaka 2018/2019.

Kauli hiyo aliitoa katika Mkutano wa Baraza la Madiwani wa kupitia taarifa ya Mthibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa hesabu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2019 uliofanyika katika ukumbi wa chuo cha Mipango Dodoma.

Dkt. Mahenge alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma imepata hati safi kwa ukaguzi wa hesabu za mwaka 2018/2019. “Niwapongeze kwa dhati kwa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa kazi nzuri mliyoifanya kwa kipindi chenu cha miaka mitano mpaka Jiji la Dodoma linapendeza, hongereni sana. Hakuna kilichotekelezwa bila kupitia vikao vya Baraza la Madiwani, Baraza hili ni sehemu ya mafanikio yote yaliyofanyika hapa Dodoma. Hamuwezi kusahauliwa katika mafanikio ya hapa Dodoma” alisema Dkt. Mahenge.

Akiongelea hoja 46 za ukaguzi zilizopatikana, Mkuu wa Mkoa aliwataka kuzitatua hoja hizo. “Ukiziangalia hoja hizi za ‘CAG’, zaidi ya asilimia 80 ninyi wenyewe mnaweza kuzitatua. Ni asilimia ndogo tu ambayo ndiyo inahitaji ngazi ya juu kama upungufu wa watumishi kwenye sekta ya afya. Mnatakiwa kuweka mkakati na ratiba ya kuhakikisha hoja zote zinajibiwa. Hoja zilizo nje ya uwezo wa Jiji niwaahidi kama serikali ya Mkoa tutaendelea kushirikiana katika kuzitatua” aliongeza Dkt. Mahenge.

Akiwasilisha taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) kwa hesabu za Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mwaka ulioishia tarehe 30 Juni, 2019, Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alisema kuwa Halmashauri ya Jiji la Dodoma ina jumla ya hoja 46 kwa mwaka 2018/2019. Katika hoja hizo, 12 ni za miaka ya nyuma na 34 ni hoja za mwaka 2018/2019. “Mheshimiwa mwenyekiti, tumeweza kupunguza hoja za ukaguzi kwa kiwango cha hoja 11 ukilinganisha na mwaka 2017/2018 ambapo tulikuwa na jumla ya hoja 57. Mheshimiwa mwenyekiti, hoja zote zimejibiwa na kuwasilishwa kwa Mkaguzi wa nje ndani ya siku 21 kama inavyotakiwa kwa mujibu wa sheria” alisema Kunambi.

Mkurugenzi huyo alisema kuwa katika ukaguzi wa hesabu za mwaka 2018/2019, Mdhibiti na Mkaguzi wa hesabu za serikali ametoa hati safi. Hati hii inalifanya Jiji la Dodoma kuendelea kupata hati safi toka mwaka 2016/2017 hadi 2018/2019.

Aidha, mwaka 2018/2019 aliutaja kuwa ni mwaka wa pekee wa kujivunia. “Nichukue nafasi hii kuipongeza kwa dhati kabisa timu yangu mahili ya wakuu wa Idara na Vitengo wa Jiji la Dodoma. Kweli wamefanya kazi nzuri. Maana msingi wa hoja unatoka kwenye idara na mimi kama afisa masuuli ninafanya matumizi ya idara zote, kama mkuu wa Idara asipokuwa makini kunishauri kwenye eneo lake tunatengeneza hoja nyingi sana. Haya ni matokeo ya kazi bora iliyotukuka” alisisitiza Kunambi.

Akiongelea siri ya Jiji kupata hati safi, Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe alisema kuwa hati safi ni ishara ya utekelezaji shughuli za maendeleo usio na shaka. “Maendeleo yanakuja mahali palipo na amani, sisi tumetulia na maendeleo yapo. Hizi hoja tunaamini zitakuwa zinabadilika kadri tunavyoendelea na zitakuwa labda zinabaki zile za kisera pakee. Nidhamu ya kutii sheria, kanuni na taratibu ndiyo msingi wa mafanikio” alisema Prof. Mwamfupe.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Dodoma mjini, Patrobas Katambi alisema kuwa mipango ya maendeleo inatolewa na serikali kupitia Ilani ya CCM na kwenye utekelezaji inaingia kwenye mfumo wa serikali wa ufuatiliaji, usimamizi na utendaji. “Ufuatiliaji na usimamizi unafanywa na Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya. Kwenye utendaji, unakuja kwenye ngazi ya Halmashauri pamoja na Baraza la Madiwani ambalo hilohilo pia linasimamia utekelezaji wake. Hivyo, hati safi maana yake ni ufuatiliaji, usimamizi na utekelezaji vinafanyika kwa usahihi” alimalizia Katambi.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.