• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Waziri Mpango apongeza wataalam Hospitali ya Mkapa

Imewekwa tarehe: February 23rd, 2021

WAZIRI wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Phillip Mpango ametokea hadharani na kuwapongeza Wataalam wa Afya katika Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa huduma bora wanazotoa hasa katika kipindi alichokuwa hospitalini hapo akipata huduma ya matibabu.

Waziri Mpango amesema “…Madaktari, manesi, wataalam wa viungo, mpaka wahudumu, yaani kila mtu wanafanya kazi usiku na mchana kwa tabasamu, kwa upendo wa ajabu, yaani huduma mimi niliyopata hapa, menejimenti ya hospitali yetu huduma hizi ndugu zangu watanzania ni huduma bora sana, sana madaktari hawa, unawaona ni vijana, sijui nitumie neno gani ‘excellent professional service’”. Alisema Dkt. Mpango kwa msisitizo.

Aidha, aliweka wazi kuwa kulikuwa na vishawishi, vya kumtaka kuhamia Dar es Salaam au mahali pengine ili akapate matibabu lakini alisema hapana. “…hakuna nilichokosa hapa kabisa kabisa, hospitali hii ni nzuri sana, vifaa ni vya kisasa kabisa, kama nilivyosema hawa ni madaktari kweli kweli, wameiva and I am proud kutibiwa na madaktari vijana wa kitanzania”.

Akifafanua Zaidi alisema kuwa sababu ya kumbilia Ulaya hata pamoja na hali ya sasa, haipo. Sisi tuelekeze nguvu kuboresha hospitali zetu hapa nchini, na amesisitiza kuwa katika nafasi ambayo Mwenyezi Mungu amemjalia kupitia uteuzi wa Rais anajisikia vizuri kwamba wakati wake kama waziri wa fedha wameweza kuelekeza fedha nyingi zaidi kuboresha huduma za afya kuanzia ujenzi wa hosptali, vituo vya afya, zahanati, dawa, kusomesha madaktari na kadharika. Dkt Mpango akasema kuwa anasikia furaha sana kwa utekelezaji huo wa Serikali.

Vile vile ameahidi kuwa kwa nafasi aliyonayo ataendelea kwa nguvu zaidi, kumshauri Mheshimiwa Rais kuelekeza nguvu zaidi na zaidi kwenye sekta ya afya ambayo inagusa sana wanyonge watanzania.

“Lazima tuboreshe zaidi bajeti ya wizara (Afya), lazima tuangalie mahitaji muhimu ya hospitali kama hii (Hospitali ya Benjamin Mkapa) iliyopo makao makuu ya nchi yetu na hospitali nyingine za hapa Dodoma, lazima tuangalie maslahi na mahitaji ya msingi ya wataalam wetu hawa wazalendo muhimu sana, manesi madaktari wote, lazima tuyaangalie upya” alisema Waziri huyo kwa kujiamini.

Akielezea Zaidi alisema kuwa kuugua kwake na kuugulia Hospitali ya Benjamin Mkaa imempa fursa na upeo katika nafasi yake ya ushauri, ya kushauri namna ambavyo kama nchi tunaweza tukafanya vizuri zaidi katika eneo la utoaji wa huduma za afya nchini.

“Nataka niwaambie watanzania afya yangu imeimarika vizuri kabisa na hatimaye jopo la madaktari wameona nina afya njema, na nina uwezo wa kurudi kuendelea na shughuli za kulitumikia taifa letu”. Alisema Dkt. Mpango kwa kujiamini.

Mwisho alitoa shukrani, kwanza ni kwa Mwenyezi Mungu aliyetuumba watu wote, kwa amemtendea makubwa, (kutoka siku 14 ambazo madaktari walikuwa wakimhudumia nyumbani na baadae wakaona wamhamishie Hospitalini Benjamin Mkapa, “acheni Mungu aitwe Mungu, tuendelee kumtukuza na kumuomba yeye aliye muweza wa yote”.

Pili kwa nafasi ya pekee sana amemshukuru sana Rais Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na familia yake, kwa kumpigia simu kila siku akimjulia hali na alikuwa akituma wasaidizi wake kufuatilia maendeleo yake siku kwa siku. Nawashukuru pia Watanzania wote na viongozi wa dini na wote.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.