• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt. Msonde aagiza mafunzo ya mfumo wa NeST

Imewekwa tarehe: March 9th, 2024

MAKATIBU Tawala wa Mikoa nchini wametakiwa kuhakikisha wakuu wa shule za msingi na sekondari na waganga wafawidhi wa vituo vya kutolea huduma za afya wanapewa mafunzo ya matumizi ya mfumo wa manunuzi (NeST) kabla ya kuanza kutumika.

Hatua hiyo inaelezwa kuwa itaongeza ufanisi katika utekelezaji wa miradi hasa ikizingatia kuwa Serikali inakusudia kupeleka fedha nyingi za miradi ya maendeleo katika maeneo hayo.

Maagizo hayo yametolewa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dkt. Charles Msonde wakati wa kufungua mafunzo ya mfumo wa ununuzi wa umma (NeST) yanayofanyika katika Ukumbi wa shule ya msingi Mtemi Mazengo Jijini Dodoma.

Alisema Serikali imekuwa ikipeleka fedha nyingi za kutekeleza miradi katika ngazi ya mzingi hivyo Ma-RAS, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa idara ya halmashauri kuhakikisha wanafundisha kwa ukamilifu wale wote wanaotekeleza shughuli za manunuzi katika ngazi ya msingi wakiwemo wakuu wa shule na waganga wafawidhi.

“Mkifanya hivyo shughuli za manunuzi zitakwenda vizuri, thamani ya fedha itaonekana kwenye miradi na itakamilika kama vile ambavyo serikali inataka.”

Pia amewataka wataalamu wote watakaohusika katika mchakato wa manunuzi kuhakikisha wanazingatia matumizi ya mfumo huo ili kujiepusha na makosa ambayo yanaweza kuwatia matatani.

Mafunzo hayo yamefanyika ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mohamed Mchengerwa ya kuhakikisha wataalamu katika serikali za mitaa wanatumia mfumo wa manunuzi wakati wa kutekeleza miradi ya ujenzi katika maeneo yao.

“Ukiwa hapa usijadili kama mtu wa Dodoma bali mwakilishe wengine ambao hawako hapa kutoka mikoa yote ya Tanzania, hivyo mnapopewa mafunzo haya myasikilize vizuri na myaelewe, palipo na utata mseme ili msije kupitisha vitu ambavyo kiuhalisia havitekelezeki,” amesema Dkt. Msonde wakati wa kusisitiza umakini wa washiriki wa mafunzo hayo.

Awali, Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Erick Kitali amesema idara yake itaendelea kuwekeza katika kuboresha na kubuni mifumo ambayo ni rafiki kwa matumizi kwa manufaa ya serikali.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.