• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dkt. Mwinyi apokea ndege mpya 2 za Tanzania

Imewekwa tarehe: October 8th, 2021

NDEGE mpya mbili aina ya Airbus A220-300, zilizonunuliwa na Serikali ya Tanzania zimewasili nchini kutokea Canada.

Ndege hizo zimepokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Sheikh Abeid Amani Karume Mjini Unguja, Zanzibar leo Oktoba 8, 2021 majira ya saa 9:00 Alasiri na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Ndege hizi ambazo zimepewa majina ya Zanzibar na Tanzanite zinakamilisha hesabu ya ndege 11 zilizonunuliwa na kuwasili hapa nchini.

Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezungumza na Watanzania katika mapokezi hayo na hapa ni baadhi ya nukuu zake.


"Wanachi wa Zanzibar wana furaha kubwa kuona kwamba tukio hili la kihistoria la kupokea ndege hizi linalofanyika hapa Zanzibar".

"Bila shaka uamuzi wa kufanya mapokezi haya Zanzibar ni kielelezo cha juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na viongozi wa taifa hili katika kuendeleza na kulinda fikra, mawazo na falsafa za waasisi wa taifa letu katika kuulinda na kuudumisha Muungano wetu".

"Mapokezi ya ndege hizi mbili aina ya Airbus ni hatua muhimu katika juhudi zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Tanzania katika kuliimarisha Shirika la Ndege la Tanzania ambalo lilianzishwa mwaka 1977".

"Sekta ya usafirishaji wa anga, majini na nchi kavu ni msingi muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa taifa letu".

"Nahimiza taasisi zetu zilizo katika viwanja vya ndege kufanya kazi kwa ushirikiano na ufanisi unaotakiwa".

"Naamini kwamba tukiwa na ndege zenye kufanya safari za moja kwa moja katika viwanja vyetu , sekta ya utalii na biashara zitaimarika kwa kasi".


Na hapa ni  nukuu za Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa.


"Leo hii ni siku ya furaha kwetu watanzania kwa mapokezi ya ndege zetu mbili mpya, ikiwa zinakamilisha ndege 11 ambazo zimenunuliwa kwa fedha yetu watanzania".

"Ununuzi wa ndege hizi ni kwa ajili ya kuongeza safari za ndani, nje na safari hizi ni kwa ajili ya kuongeza fursa kujiongezea uchumi wa taifa au wa mtu mmoja mmoja kwa wale ambao wataamua kufanya biashara zao kupitia ndege hizi".

Aliyosema Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa

"Kuwasili kwa ndege izi mbili kutaifanya ATCL kuendelea kutoa huduma za uhakika, kuongeza miluko kwa safari za ndani,na kuweza kuanzisha safari mpya za kikanda katika miji mikuu ya biashara ikiwemo kinshasa,lubumbashi,Nairobi na Ndola".


Nukuu za Mkurugenzi mtendaji wa ATCL Injinia Ladislaus Matindi

"Ndege zedtu zimeletwa na marubani wetu wenyewe na waandisi na wote waliohusika katika makabidhiano na ukaguzi wa ndege wote ni watanzania tofauti na miaka iliyopita".

"Ndege hizi mbili zilizokuja leo ni toleo jipya ambalo tumeboresha baadhi ya vitu kutokana na mahitaji katika soko na zitatuweka katika hali nzuri ya ushindani".

"Ndege izi zina uwezo wq kubeba abiria 132 kila moja,ambapo abiria 12 wako katika daraja la biashara na abiria 120 katika daraja la uchumi na inaruka saa 6 bila kutua ikiwa na abiria na mizigo".

"Imewekewa mifumo ya kuwasaidia marubani kuruka na kutua ili kuongeza ufanisi katika utendaji wao wa kazi".


"Pia zimeongezwa kiasi cha kubeba uzito wakati wa kuruka kutoka tani 67.6 hadi tani 69.9".


"Ndege izi zimewekwa mifumo ya burudani zikijumuisha sinema za watoto,michezo ya watoto, vichekesho, miziki na mitandao ya internet (wi-fi)".

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuashiria kupokea na kuzindua ndege mpya mbili aina ya Airbus A220-300 kwa ajili ya kutoa huduma kwa wateja wa ATCL.


Chanzo: Idara ya Habari Maelezo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.