• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Dodoma, fursa mpya kwa uchumi wa Tanzania, wekeza Dodoma, Tukufanikishe"

Imewekwa tarehe: June 27th, 2019

MKOA wa Dodoma umeandaa kongamano la uwekezaji kwa ajili ya kutangaza fursa za uwekezaji zilizopo kwa lengo la kuvutia wawekezaji katika maeneo mbalimbali na kukuza uchumi wa mkoa huo.

Kauli hiyo ilimetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge alipokuwa akitoa maelezo muhimu kuhusu Kongamano la Uwekezaji la Mkoa wa Dodoma kwa mgeni rasmi Waziri Mkuu wa Tanzania katika ukumbi wa Dodoma Convention Centre.

Dkt. Mahenge alisema “katika kufikia azma ya serikali ya kujenga uchumi wa viwanda, Mkoa wa Dodoma umeandaa kongamano hili la uwekezaji kwa lengo la kutangaza fursa na vivutio vya uwekezaji vilivyopo katika Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi”.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa Mkoa wa Dodoma unazo sifa zinazoufanya uvutie kwa uwekezaji. Sifa hizo alizitaja ni kuwa makao makuu ya serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. “Fursa kubwa ya uwepo wa soko la bidhaa mbalimbali zitakazozalishwa hapa na soko kubwa la mahitaji ya huduma za jamii kutokana na idadi kubwa ya watu wanaohamia Dodoma wenye kipato cha kati na kikubwa. Wageni kutoka mataifa mbalimbali, mabalozi na taasisi za kimataifa. Fursa nyingi za uwekezaji na biashara kwenye ujenzi wa makao makuu mapya ya nchi katika karne ya 21 ya sayansi na teknolojia za kisasa” alisema Dkt. Mahenge. Wawekezaji na wafanyabiashara hawahitaji kufanya utafiti wowote ili kufanya biashara kutokana na ukweli kwamba makao makuu ya nchi mahitaji ya hoteli za kisasa, nyumba za wageni, huduma za afya za kisasa na shule za kimataifa hayakwepeki, aliongeza.

“Napenda kwa niaba ya serikali, Mkoa na wananchi  kutoa pongezi na shukurani kwa Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uamuzi wake thabiti wa kuhamishia makao makuu ya serikali mkoani Dodoma, jambo ambalo ni kichocheo na chanzo kikuu cha fursa nyingi za uwekezaji” alisema Dkt. Mahenge.

Akiongelea uboreshaji mazingira ya uwekezaji mkoani Dodoma, Mkuu wa Mkoa alisema kuwa Kituo cha Uwekezaji Tanzania  (TIC) kimefungua ofisi ya kanda ya kati jijini Dodoma.

“Huduma mbalimbali zikiwepo kupata taarifa na taratibu za uwekezaji, maombi ya vibali na leseni mbalimbali za uwekezaji kwa wawekezaji wanaowekeza Dodoma zinaratibiwa na ofisi hii. Wawekezaji wa ndani na nje wamechangamkia fursa hii ambapo kwa kipindi cha mwezi Julai 2016 hadi Juni 2019, jumla ya miradi mipya 22 imesajiliwa katika Mkoa wa Dodoma ambayo inatarajia kuwekeza mtaji wa Dola za Marekani 232.51 Milioni na kuzalisha ajira mpya 2,867” alisema Dkt Mahenge.

Suala la usafiri si kikwazo kwa Mkoa wa Dodoma. Alisema kuwa mkoa huo umeunganishwa na miundombinu ya usafiri na usafirishaji mizuri kwa barabara za lami zinazounganisha na mikoa mingine, na kiwanja cha Ndege. “Ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji unaendelea sasa: SGR, barabara za pete ya ndani na nje, uwanja wa kimataifa wa ndege Msalato, stendi ya kisasa na soko” alisisitiza Dkt. Mahenge.

Kongamano la Uwekezaji Mkoa wa Dodoma litafanyika kwa siku mbili likiongozwa na Kaulimbiu isemayo “Dodoma fursa mpya ya kiuchumi Tanzania, wekeza Dodoma, tukufanikishe”.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.