• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mazingira ni agenda inayosababisha uchumi kuwa imara - Waziri Jafo

Imewekwa tarehe: February 7th, 2022

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Dkt. Selamani Jafo amesema mazingira ndiyo ajenda inayosababisha uchumi kuwa imara.

Amesema hayo wakati akizungumza na wanafunzi kutoka shule mbalimbali, viongozi na wananchi walioshiriki zoezi la upandaji miti katika eneo la Medeli jijini Dodoma leo Februari 7, 2022.

Dkt. Jafo alisema kuwa uchumi imara ni matokeo ya utunzaji mazingira kwa kuwa ni chanzo cha mvua ambazo zinasaidia kujaa kwa maji katika mabwawa ya kufua umeme ambao hutumika katika viwanda.

“Ndugu zangu tukikosa mvua tutakosa umeme na tukikosa umeme viwanda vitashindwa kufanya kazi na vikishindwa kufanya kazi watu watakosa ajira na watu wakikosa ajira uchumi utaporomoka kwa hiyo agenda ya mazingira inasababisha hata uchumi kuweza kuwa imara,” alisema.

Zoezi hilo ambalo ni miongoni mwa shughuli zinazofanyika kuelekea uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021 unaotarajiwa kufanywa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango Februari 12, 2022.

Pia, Waziri Dkt. Jafo alitumia nafasi hiyo kutoa rai kwa wananchi kutumia mvua zinazonyesha katika maeneo mbalimbali nchini kupanda miti ili ikue na ambayo itasaidia katika kurejesha mazingira katika hali nzuri.

Aliwashukuru wadau mbalimbali waliojitokeza na kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais wakiwemo Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wanafunzi na wananchi kwa ujumla kushiriki katika zoezi hilo.

Aidha, waziri huyo alihamasisha wanafunzi hao kupeleka ujumbe kwa wazazi wao kushiriki katika zoezi la kupanda miti katika maeneo yao ili kuifanya Dodoma kuwa ya kijani.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi. Mary Maganga alisema katika zoezi hilo wameweza kupanda aina mbalimbali za miti ikiwemo ya matunda na kivuli.

Bi. Maganga alisema kuwa zoezi hilo limekwenda vizuri na watu wamejitokeza kwa wingi kushiriki kupanda miti pamoja na kuwepo kwa changamoto ya kuwepo kwa mvua.

Serikali imeamua kuwa na Wiki ya Uzinduzi wa Sera iliyoanza leo Februari 7, 2022 ambayo inaambatana na shughuli mbalimbali za hifadhi ya mazingira ikiwa ni sehemu ya masuala ya msingi yanayoelekezwa katika Sera mpya.

Ikumbukwe kwamba Sera ya Taifa ya Mazingira ya Mwaka 2021 imeongeza wigo wa masuala na changamoto za mazingira zinazopaswa kufanyiwa kazi katika kipindi husika ili kuleta maendeleo endelevu na imezingatia changamoto mpya za kimazingira zinazoendelea kujitokeza kutokana na mabadiliko ya mifumo ya kiuchumi, kijamii na kimazingira yanayoendelea duniani.

Dhumuni la kuwepo kwa shughuli hizo ni kurejesha hali ya asili ya mazingira iliyoharibika kutokana na shughuli za kibinadamu kwa kuwa na zoezi la upandaji miti, kuboresha afya ya jamii na elimu ya utenganishaji taka kwa ajili ya udhibiti wa taka ngumu na kuwezesha urejelezaji wa taka kwenye bidhaa na huduma mbalimbali.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.