• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Mkataba wa ununuzi wa behewa 1430 za mizigo za reli ya kisasa – SGR wasainiwa

Imewekwa tarehe: February 8th, 2022

Shirika la Reli Tanzania – TRC limesaini mkatabana kampuni ya CRRC International kutoka nchini China kwa ajili ya ununuzi waBehewa 1430 za mizigo zitakazotumika katika reli ya kisasa – SGR, hafla yautiaji saini imefanyika katika ukumbi wa mikutano makao makuu TRC Februari 08,2022.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi wa Serikalina Shirika, ambapo Mgeni Rasmi katika hafla hiyo alikuwa Waziri wa Ujenzi naUchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TRC,Mkurugenzi Mkuu TRC, Wawakilishi wa kampuni ya CRRC International, Menejimentina Wafanyakazi wa TRC pamoja na wanahabari.

Mhe. Prof. Makame Mbarawa, Waziri wa Ujenzi naUchukuzi ameshuhudia zoezi la utiaji saini mara baada ya kupata taarifa fupi yamkataba wa ununuzi wa behewa hizo pamoja na maendeleo ya ujenzi wa reli yakisasa nchini kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa TRC Ndugu Masanja Kungu Kadogosakuwa Ujenzi wa reli ya kisasa unaoendelea kwa sasa ni kipande cha Dar es Salaam– Morogoro umefika 95%, Morogoro – Makutupora umefika 81% na Mwanza – Isakaumefika 4%.

Hata hivyo Waziri Mbarawa alisema kuwa katikaBehewa hizo 1430 zitakazotengenezwa zipo Behewa 60 za mifugo ambapo Behewa mojaitakuwa na uwezo wa kubeba takribani Ngo’mbe 100 ambayo ni sawa na Ngo’mbe6,000 kwa behewa 60. Pia zipo behewa 50 maalumu kwa ajili ya kubeba magariambapo behewa moja itakuwa na uwezo wa kubeba magari madogo 8 ambayo ni sawa namagari 400 kwa behewa 50.

Mhe. Waziri alifafanua kuwa “kutokana na uwezomkubwa wa reli ya kisasa, behewa hizi zitasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguzamrundikano wa mizigo katika bandari ya Dar es Salaam ambapo treni moja itakuwana uwezo wa kubeba Tani 10,000 kwa mkupuo ambayo ni sawa na malori 500” alisemaProf. Mbarawa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Waziri aliwapongezawafanyakazi wa Shirika la Reli kwa usimamizi mzuri wa mradi wa ujenzi wa reliya kisasa na kuwaomba waendelee kuchapa kazi kwa kutumia weledi walionao najitihada ili kutimiza malengo ya Serikali ya kuhudumia wananchi na kukuzauchumi wa Taifa.

Mkurugenzi Mkuu TRC, Ndugu Masanja Kadogosakatika taarifa yake amesema kuwa,
“Mkataba huu ni wa ununuzi wa behewa 1430 za mizigo za reli ya kisasa ambaounagharimu Dola za Kimarekani Milioni 127.2, ni mkataba wa miezi 12 yaani mwakammoja utakaohusisha usanifu na utengenezaji wa behewa kwa ajili ya kubebamizigo ya aina mbalimbali kulingana na aina ya behewa na matakwa ya mteja kupitiareli ya kisasa”.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkurugenzi mkuualiweka wazi kuwa aina ya behewa zitakazonunuliwa kupitia mkataba huu ni,behewa 600 aina CCB (Container Carrier Bogie) kwa ajili ya kubeba makasha,behewa 400 aina ya CLB (Covered Large Bogie) kwa ajili ya kubeba mizigo yajumla ikiwemo Sukari, Saruji, Chumvi, Pamba, Tumbaku na Kahawa, behewa 190 ainaya PTB (Petroleum Tank Bogie) kwa ajili ya kubeba mafuta aina zote, Behewa 70aina ya HLB (High Large Bogie) kwa ajili ya Mabomba, Mbao, Magogo na Vyuma,behewa 50 aina ya MGB (Motor Goods Bogie) kwa ajili ya kubeba magari na behewa50 aina ya CWB (Cattle Wagon Bogie) kwa ajili ya kubeba Ng’ombe.

Kwa upande wake Mwakilishi wa kampuni ya CRRCambaye ni Meneja Msaidizi Bw. Tang Yun Peng amesema kuwa “Leo ni siku nzurikwetu CRRC kwa sababu haikuwa rahisi kufikia hapa, nakumbuka mwaka janatulishiriki katika mradi wa uboreshaji wa reli ya kati, hivyo tuna ujasiri wakutosha kusanifu na kutengeneza behewa bora na imara kwa ajili yenu” alisemaBw. Peng.

Shirika la Reli Tanzania linatarajia kukamilikakwa manunuzi na kuwasili kwa behewa hayo mapema Februari 2023 ambako kutakwendasambamba na kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa reli ya kisasa kipande cha piliMorogoro – Makutupora ambacho kwa umbali huo kutaweza kuleta tija na faidakatika uendeshaji wa huduma ya usafirishaji mizigo.

Chanzo: Tovuti ya TRC

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.