• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Diwani Ngede, wazazi 'waifagilia' serikali ukarabati shule

Imewekwa tarehe: February 26th, 2022

WAZAZI na walezi wa kata ya Chamwino Jiji la Dodoma, wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa hatua yake ya kutoa fedha kupitia Halmashauri ya Jiji, kiasi cha milioni 59, kwa ajili ya ukarabati wa vyumba sita vya madarasa vinavyovuja na kusababisha wanafunzi na walimu kunyeshewa na mvua na kushindwa kusoma na kufundisha.

Shukrani hizo zilitolewa na wazazi na walezi hao mbele ya Naibu Meya wa Jiji la Dodoma Emmanuel Chibago,walipokuwa wakizungumza kwenye kikao cha mkutano wa hadhara wa kujadili maendeleo uliofanyika shule ya msingi Chamwino (A) Dodoma.

Asha Ramadhani, Mariam Hassani wakizungumza kwa niaba ya wazazi na walezi wezao kwenye kikao hicho cha maendeleo cha shule, walisema kuwa fedha zilizotolewa na serikali kwa kupitia Jiji la Dodoma,zitakuwa mkombozi kwa wanafunzi na walimu ambao kwa kipindi kirefu wananyeshewa wanapokuwa kwenye madarasa hayo ambayo mabati yeke ni machakavu.

“Tuna kila sababu ya kuishukuru Rais kwa kutoa kiasi hicho cha fedha cha milioni 59 kwa ajili ya ukarabati wa majengo hayo ya shule,hivyo ni imani yetu sisi kama wazazi wanafunzi wetu na walimu wetu, watakuwa sehemu salama na hata ufaulu sasa utaongezeka zaidi”Maliam alisema.

Awali akizungumza kwenye mkutano huo wa wazazi na walezi Diwani wa kata ya Chamwino Jiji la Dodoma,Jumanne Ngede,alisema kuwa kwa muda mrefu vyumba hivyo vya madarasa yapatayo sita ni machakavu na yanavuja ,kwa maana hiyo kupatikana kwa fedha hizo kero hiyo inaenda kutatuliwa .

“Ni imani yangu sasa wanafunzi watasoma mahali salama, walimu watafundisha kwa uhuru, na ufaulu utaongezeka zaidi,hivyo niwaombea wale wote watakaohusika na ukarabati fedha zitumike kwa malengo yaliyokusudia ukizingatia kuwa Rais Samia ameipa heshima Halmashauri kutupatia fedha hizo” alisema.

Hivyo wazazi na walezi mnatakiwa kuiunga mkono serikali chaini ya Rais Samia Suluhu Hassan kutokana na juhudi kubwa zinazowekezwa kwenye elimu,kwa maana hiyo ninawaomba mshiriki katika kujitoa kuhakikisha ukarabati wa majengo hayo unafanyika kwa haraka na kwa uaminifu mno.

Diwani huyo amewataka wazazi kuhakikisha wanachangia kwa nguvu kazi pindi kwenye ukarabati huo utakapowadia ili wanafunzi na walimu waweze kuondokana na hadha inayowapata kwa kipindi hiki cha mvua zinazoendelea kunyesha ili kuiunga serikali ambayo imetoa fedha hizo kupitia halmashauri ya Jiji.

Kwa upande wake Naibu Meya ya Jiji la Dodoma Emmanuel Chibago akizungumza na wazazi na walezi wa kata hiyo ya Chamwino (A) ameiagiza kata na uongozi wake, kuhakikisha ukarabati huo unaanza mara moja ili kulitatua suala hilo lililopo kwenye shule hiyo ambayo majengo yake yanavuja .

Chibago alisema kuwa serikali kupitia Halmashauri ya Jiji bado itaendelea kuisaidia shule hiyo kwa kushirikiana na wazazi na walezi katika kutatua kero,hivyo niwataka kujitokeza kwa wingi kushiriki ili wanafunzi na walimu wawe salama kwenye maeneo husika.

Alisema kuwa shule ya msingi ya Chamwino serikali kupitia halmashauri inatambua kuwa ina mapungufu mengi,ikiwemo vyoo na madawati,hivyo hatuwezi kufuta siro wakati inakabiliwa na changamoto hizo hivyo ni lazima wazazi na walezi washirikiane katika kutatua kero hizo.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.