• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

'CHF iliyoboreshwa' yapokelewa kwa shangwe Chang'ombe

Imewekwa tarehe: December 15th, 2019

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imesajili wanachama 330 katika siku yake ya kwanza ya utekelezaji wa zoezi maalum ya uhamasishaji wananchi kujiunga na Bima ya Afya ya Jamii iliyoboreshwa (CHF) katika Kata ya Chang’ombe mwishoni mwa wiki hii.

Akizungunza na wanahabari baada ya zoezi hilo mratibu wa CHF iliyoboreshwa Patrick Sebyiga alisema kuwa zoezi hilo limeanza kwa mafanikio makubwa katika Kata ya Chang’ombe kutokana na mwitikio wa wananchi kuwa mzuri.

Sebyiga alisema kuwa idadi ya kaya zilizosajiliwa ni 55, zenye jumla ya watu 330. “Katika Kata ya Chang’ombe muitikio wa watu ni mkubwa na hii imetupa picha kuwa zoezi la usajili linatakiwa kuendelea katika Kata hiyo” alisema Sebyiga.

Mratibu huyo alisema kuwa hoja nyingi za wananchi zilikuwa zinajikita katika iliyokuwa CHF ya awali. “Timu yangu ya wataalam na wahamasishaji imeendelea kuwaelimisha wananchi tofauti ya CHF ya awali na CHF hii iliyoboreshwa na baada ya kuelewa wananchi wamekuwa wakijiunga” alisema mratibu huyo.

Akiongelea tofauti baina ya CHF ya awali na iliyoboreshwa, alisema CHF iliyoboreshwa huduma zake zimeboreshwa. “CHF ya awali ilikuwa usajili unafanyika kwa kujaza fomu na baada ya hapo unasubiri mwezi mmoja ndipo uanze kupata huduma ya matibabu. Kwa CHF iliyoboreshwa ni ya kidigitali ambayo usajili na kadi yako unapewa papohapo na huduma ya matibabu kuanza mara moja” alisema Sebyiga.

Tofauti nyingine aliitaja kuwa CHF iliyopita walengwa wengi walikuwa hawapati huduma ya tiba na dawa katika vituo vya afya. “Sasa huduma zimeboreshwa zaidi. Matibabu hutolewa kuanzia ngazi ya Zahanati. Pale ambapo mgonjwa anahitaji rufaa basi utaratibu wa rufaa hufanyika kwenda kituo cha Afya, Hospitali ya Wilaya hadi hospitali ya rufaa ya Mkoa. Hii yote ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. John Magufuli za kumhakikishia mwananchi huduma bora za matibabu. Matibabu sasa ni nchi nzima katika vituo vya afya na hospitali za serikali” alisema Sebyiga.

Mratibu huyo alisema kuwa zoezi la uhamasishaji ni endelevu litakalofanyika katika Kata zote 41 za Halmashauri ya Jiji la Dodoma.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.