• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma Jiji FC 'kusaka' historia kesho

Imewekwa tarehe: July 10th, 2020

TIMU ya soka ya Dodoma Jiji FC iliyo chini ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kesho Jumamosi Julai 11, 2020 itatupa karata ya kihistoria katika uwanja wa Jamhuri Jijini humo ambayo itaamua endapo timu hiyo itafuzu moja kwa moja kupanda Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara inayodhaminiwa na kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom kwa msimu ujao au vinginevyo kwa kukabiliana na Iringa United ya mkoani Iringa.

Mchezo huo wa mwisho wa ligi daraja la kwanza kwa msimu huu unatarajiwa kupigwa saa 10:00 jioni, na unatarajiwa kutoa hatma ya Dodoma Jiji FC kwani ili ifuzu italazimika kushinda ili kujihakikishia kupanda Ligi Kuu msimu ujao na endapo itapoteza itasubiri kupata matokeo ya mchezo mwingine wa kundi A kati ya Ihefu FC ya Mbarali Mbeya itakayokuwa kibaruani dhidi ya Cosmopolitan ya Dar es Salaam kwenye dimba la Highland Estates lililopo katikati ya mashamba ya mpunga huko Ubaruku Wilayani Mbarali Mkoa wa Mbeya.

Mpaka sasa Dodoma Jiji inaongoza kundi mbele ya Ihefu kwa tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa huku timu zote zikiwa na pointi 48, hali iliyopelekea ushindi wa aina yake katika kundi hilo mpaka hapo michezo ya mwisho inayopigwa mwishoni mwa wiki hii itakapoamua mbivu na mbichi tofauti na kundi B ambapo timu ya Gwambina FC ya Misungwi mkoani Mwanza ilishafuzu kucheza Ligi Kuu msimu ujao ikiwa na michezo kadhaa ‘mkononi’.

Akizungumzia mchezo wa kesho, Afisa Habari Dodoma Jiji FC Ramadhani Juma amesema kikosi chao kimeandaliwa vizuri kimwili na kiakili kuhakikisha kinawapa raha wana Dodoma baada ya kukosa uhondo wa Ligi Kuu kwa takrabani misimu nane katika Jiji hilo.

“Kocha Mkuu Mbwana Makata akishirikiana na wasaidizi wake Renatus Shija na Mfaume Athumani wamekiandaa kikosi tayari kwa ‘vita ya kesho, ni mchezo wa kihistoria ambao utairudisha Dodoma kwenye ligi kuu ya Tanzania” alisema Juma.

Alisema maandalizi yote ya mchezo huo yamekamilika na kinachosubiriwa ni muda tu, na kwamba ushirikiano  wa wadau wote ni muhimu katika kipindi hiki ili kufikia lengo la kupanda daraja kwa timu hiyo.

“Kwanza kwa niaba ya uongozi na Halmashauri ya Jiji kwa ujumla nitoe shukran nyingi sana kwa wapenzi na wadau wa timu na wakazi wote wa Dodoma kwa ushirikiano na mapenzi makubwa waliyoyaonesha kwa timu yao tangu mwanzo wa ligi, tumefika hapa leo kwa juhudi na ushauri wao katika kuiunga timu mkono” alisema.

Juma alitoa wito kwa wakazi wa Dodoma na Wilaya zake kufurika kwa wingi kesho kwenye uwanja wa Jamhuri ili kukamilisha kazi waliyoianza Septemba mwaka jana.

“Ni mchezo wa kihistoria hivyo nadhani kila mwana Dodoma ahakikishe anakuwa sehemu ya historia hiyo kwa kuja uwanjani ili kuwapa nguvu ya kupambana wachezaji wetu ambao wamekuwa wakipigana katika mchezo kwa nguvu zao, mchezo utaanza saa kumi kamili jioni na kiingilio itakuwa shilingi elfu (2,000) tu” alisistiza.

Timu hiyo ilichukuliwa na Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoka wadau ambao walipambana kuipandisha daraja kwa misimu miwili iliyopita lakini hawakufanikiwa.  



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.