• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma Jiji, Mbeya City hakuna mbabe

Imewekwa tarehe: October 16th, 2020

NDUGU wawili Dodoma Jiji FC na Mbeya City FC zimegawana pointi moja moja baada ya kutoka suluhu ya bila kufungana katika mchezo wa duru la sita la Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, mchezo uliochezwa katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma.

Dodoma Jiji FC, Mbeya City na KMC ni timu ambazo ziko Ligi Kuu na zote zinamilikiwa na Halmashauri za maeneo yao. Huu ni mchezo wa kwanza Dodoma Jiji inakosa kupata ushindi katika uwanja wake wa nyumbani. Dodoma Jiji FC ilipata ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza dhidi ya Mwadui FC, ikaishinda JKT Tanzania 0-2 katika uwanja huo huo (ambapo yenyewe ilikuwa ugenini) na ikarejea kama mwenyeji kwenye mchezo na Ruvu JKT na kushinda bao 2-0.

Dodoma Jiji FC inafikisha jumla ya alama 11 ikishika nafasi ya 5 kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara ikitanguliwa na vinara Azam FC (18), Simba SC (13), Yanga SC (13) na Biashara United FC (13).

Mbeya City FC wako nafasi ya 18 na alama zao 2 tu wakiwa wameshuka dimbani mara sita na kuambulia sare 2 (kwenye mchezo na Tanzania Prisons na leo dhidi ya Dodoma Jiji FC), na hawana goli hata moja.

Dodoma Jiji FC sasa watasafiri kwenda Kagera kwenye uwanja wa Kaitaba Bukoba kupambana na timu nyingine kongwe ya Ligi Kuu inayosuasua 'wakata miwa' wa Kagera Sugar Oktoba 20.

Katika mchezo wa leo Dodoma Jiji FC iliwakilishwa na Aron Kalambo, George Wawa, Abubakari Ngalema, Mbwana Kibacha (Nahodha), Augustino Samson, Rajab Mgalula, Dickson Ambundo, Cleophace Mkandala, Anuary Jabiri, Khamis Mcha na Jamal Mtegeta, na wachezaji wa akiba walikuwa Emmanuel Mseja, Anderson Solomon, Hassan Kapona, Steven Mganga, Omary Kanyoro, Santos Thomas na Peter Mapunda

Kila la heri Dodoma Jiji FC katika mchezo unaofuata. "Timu yetu, Jiji letu"

Manahodha wa Dodoma Jiji FC Mbwana Kibacha (jezi Namba 15) na Mpoki Mwakinyuke wa Mbeya CIty FC wakisalimiana kabla ya mchezo kati ya timu zao.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.