• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Jiji lapambana kuangamiza Mbu, Malaria haikubaliki

Imewekwa tarehe: October 2nd, 2020

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeendelea kufanya afua ya upuliziaji wa viuadudu vya kuangamiza viluwiluwi wa mbu waenezao ugonjwa wa Malaria kwa awamu ya tatu, zoezi  lililoanza tarehe 28/09/2020 na kukamilika leo 02/2/2020.

Ikumbukwe kuwa tarehe 22 Juni, 2017 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli alizindua rasmi upuliziaji wa viuadudu katika maeneo yote nchini ili kutokomeza Mbu waenezao Malaria.

Aidha, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Ummy Mwalimu aliwatangazia Wakurugenzi  wa Halmashauri zote nchini kutekeleza zoezi la kuchukua viuadudu hivyo ili kupunguza kiwango kikubwa cha maambukizi ya ugonjwa wa Malaria mara zoezi la utekelezaji litakapokamilika.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma hadi sasa imepokea jumla ya lita 21,360 ambapo lita20,480 zilipokelewa awamu ya kwanza mwaka 2017 na lita 880 zilipokelewa mwaka 2020 na zote kwa pamoja zimepulizwa katika maeneo mbalimbali ya mazalia ya Mbu katika Jiji la Dodoma.

Naye Afisa Afya wa Jiji la Dodoma Abdallah Mahia amewasisitiza wataalam kufanya upuliziaji wa viuadudu kwa kuzingatia miongozo na Wizara ya Afya kama inavyofanyika jijini hapa. Hii itawezesha kupata matokeo tarajiwa ya kutokomeza Mbu ili kudhibiti ugonjwa wa Malaria nchini.

Mahia amesema hadi sasa Kata zilizofikiwa na zoezi hili ni Miyuji, Ntyuka, Nzuguni, Nkuhungu, Madukani, Chamwino, Kiwanja cha Ndege, Mnadani, Msalato, Matumbulu, Hombolo, Ipagala, Hazina na Dodoma Makulu.

Vilevile, baadhi ya wananchi waishio Jijini Dodoma waliotakiwa kutoa maoni yao kuhusiana na zoezi hili wamemshukuru na kumpongeza kwa dhati Mhe. Dkt. John Magufuli kwa kutekeleza kwa vitendo mapambano dhidi ya Malaria nchini.

Anna Makali mkazi wa Kata ya Msalato alisema "kwa kweli tunamshukuru sana Rais wetu Magufuli kwa kusaidia hadi Serikali imetoa madawa haya ya kuua mazalia ya Mbu kwenye mitaa yetu. Kwa kweli mimi binafsi na watu wote hapa tunampongeza sana"

Aidha, wamemshukuru Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru na Halmashauri ya Jiji hili kwa jitihada zinazochukuliwa na Jiji hili kutekeleza zoezi hili muhimu.

Afisa Afya wa Jiji la Dodoma Abdallah Mahia alipokuwa akielezea juu ya zoezi la upuliziaji wa viuadudu vya kuangamiza viluwiluwi wa mbu waenezao ugonjwa wa Malaria Jijini Dodoma.







Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.