• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma Jiji, Mamlaka Ngorongoro wakubaliana kuboresha Mji, Utalii

Imewekwa tarehe: July 2nd, 2018

HALMASHAURI ya Jiji la Dodoma imeingia makubaliano ya utunzaji na upambaji wa maeneo ya barabara yenye mizunguko (round about) na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCA), ambapo Mamlaka hiyo itahudumia maeneo hayo kwa kutunza bustani za maua na kuweka sanamu za wanyama ikiwemo Tembo.

Hafla ya kusaini hati ya makubaliano imefanyika leo Julai 2, 2018, katika Ukumbi mdogo wa Mikutano wa Jiji la Dodoma na kuhudhuriwa na Mstahiki Meya wa Jiji hilo Profesa Davis Mwamfupe na Mkurugenzi wa Jiji Godwin Kunambi, huku Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ikiwakilishwa na Ofisa Uhusiano Mkuu wa Mamlaka hiyo Joyce Mgaya kwa niaba ya Mhifadhi.

PICHA: Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Godwin Kunambi (kulia) akimkabidhi hati ya makubaliano Ofisa Uhusiano Mkuu wa Mamlaka ya Uhifadhi ya Ngorongoro Joyce Mgaya kwa niaba ya Mhifadhi, mara baada ya kutiliana saini makubaliano ya kuboresha Mazingira ya Mji wa Dodoma na kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo Nchini.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo iliyohudhuriwa pia na Waandishi wa Habari wa Vyombo mbalimbali, Mkurugenzi Kunambi alisema wamekubaliana kuwa, maeneo matatu ya mizunguko yatakabidhiwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, ambapo moja lipo barabara ya Dodoma-Dar es Salaam eneo la Ipagala, jingine lipo barabara ya Dodoma-Singida, na eneo la tatu ni mzunguko uliopo barabara ya Dodoma-Babati jirani na uwanja wa ndege.   

PICHA: Mkuu wa Idara ya Mazingira na Udhibiti wa Taka Ngumu Dickson Kimaro akifafanua baadhi ya mambo kwa Waandishi wa Habari wakati wa makabidhiano ya maeneo ya mizunguko ya barabara katika Mji wa Dodoma yatakayoboreshwa na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro ambapo pia yatatumika kutangaza vivutio vya Utalii vilivyopo Nchini.


Kwa upande wake, mwakilishi wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro Joyce Mgaya alisema baada ya kukabidhiwa maeneo hayo na Jiji la Dodoma, Mamlaka itaanza mara moja kazi ya kuyaboresha na kuweka sanamu za baadhi ya wanyama wanaopatikana katika hifadhi hiyo ili kuufanya Mji wa Dodoma kuvutia zaidi na kutangaza vivutio vya utalii vilivyopo Nchini.

Kwa upande wake, Mstaki Meya Profesa Mwamfupe alisema Mji wa Dodoma unahitaji juhudi za Jiji na wadau mbalimbali kuupendezesha kwa kuzingatia kuwa ndiyo Makao Makuu ya Nchi, huku akitoa wito kwa wakazi wa Jiji hilo kudumisha usafi wa mazingira kwenye makazi yao na maeneo ya biashara ili Mitaa yote ya Mji wa Dodoma iwe safi muda wote.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.