• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma kuandika historia, kuapishwa kwa Rais

Imewekwa tarehe: November 4th, 2020

HISTORIA mpya inatarajiwa kuandikwa kesho tarehe 5.11.2020 kwa wakazi wa Mkoa wa Dodoma kushuhudia sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mara ya kwanza tangu kupata Uhuru.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge katika mkutano wake na waandishi wa habari Jijini Dodoma, alipokua akizungumzia kuhusu maandalizi ya sherehe hizo ambazo wakazi wa Dodoma na Watanzania kwa ujumla watashuhudia kuapishwa kwa Rais mteule Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Jamhuri Jijini hapa.

Dkt. Mahenge amesema kuwa ni heshima kubwa kwa Mkoa wa  Dodoma kupata fursa ya kushuhudia tukio hilo la kistoria ambalo hufanyika mara moja ndani ya miaka mitano na anaamini kuwa limeleta mianya ya biashara na kuinua uchumi ndani ya Mkoa wa Dodoma.

“Haya ni matunda makubwa ya uamuzi wa Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wa kuhamishia Makao Makuu ya Serikali Mkoani Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa ndoto ya Baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyerere aliyoanza kuitekeleza mwaka 1973”, Alisema Dkt. Mahenge.

Amesema kuwa matukio makubwa kama haya yatakuwa yakifanyika Mkoani Dodoma na kutoa fursa na hamasa kwa wawekezaji kama vile wa huduma za usafiri, mahoteli, nyumba za kulala wageni, kumbi za burudani, mama lishe, machinga na wengine wengi.

Hata hivyo Dkt. Mahenge ametoa rai kwa wanachi wa Dodoma kutokua sehemu ya bugudha na usumbufu kwa wageni wanaokuja licha ya kuwa Dodoma ni sehemu yenye amani wakati wote hivyo amewataka kuimarisha na kudumisha sifa hiyo ikiwa ni pamoja na kuboresha viwango vya huduma na biashara zao.

“Sherehe hizi zitahudhuliwa na Marais na viongozi wa juu kutoka mataifa mbalimbali, viongozi wastaafu na wafanyabisha wakubwa hivyo tukiboresha huduma katika biashara zetu tutawavutia kurudi tena hata baada ya zoezi hili kuisha kwa ajili ya kutembea na kufanya uwekezaji mbalimbali” Aliongeza Dkt. Mahenge.

Aidha Dkt. Mahenge amesema kuwa sherehe hizo zitapambwa kwa burudani mbalimbali ikiwa ni pamoja na gwaride maalum lililoandaliwa na vikosi mbalimbali vya ulinzi vya Tanzania, vikundi vya ngoma, Pamoja na wasanii wa kizazi kipya kama vile Halmonize, Zuchu, Nandy, Sholo Mwamba na Dulla Makabila.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amewakaribisha na kuwahimiza wananchi wote kuwahi kufika uwanjani mapema ili kuepuka usumbufu na kuongeza kuwa milango itakua wazi kuanzia saa 12 alfajiri.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.