• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma liwe Jiji safi, la kisasa - RC Mtaka

Imewekwa tarehe: June 16th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

WANANCHI wa Dodoma wametakiwa kuwa na utamaduni kuheshimu na kutunza usafi wa mazingira ili kulifanya Jiji la Dodoma kuwa safi na la kisasa.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka katika hafla fupi ya ugawaji vifaa vya kuhifadhi taka katika bustani ya Nyerere square jijini Dodoma.

Mtaka alisema kuwa wananchi wa Dodoma lazima wawe na utamaduni wa kupenda usafi. “Namna bora ya kuwasaidia ni kwenda kwenye adhabu. Naibu Meya upo hapa, tuharakishe mchakato wa sheria ndogo zinazohusiana na usafi wa mazingira” alisema Mtaka.

Aliwataka wananchi kuacha tabia ya kutupa taka ovyo. Alisema kuwa mitaro mingi ni michafu katika Halmashauri ya Jiji. Aliagiza mitaro hiyo kusafishwa ili iweze kutumu na kufanya kazi iliyokusudiwa. 

Aidha, alikemea tabia ya viwanja kutekelezwa bila kufanyiwa usafi. “Dodoma hatuhitaji viwanja pori, vinafuga wezi. Fyeka majani kwenye kiwanja chako na panda miti” alisema Mtaka.

Kwa upande wa Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya NMB, Juma Kimori alisema kuwa benki yake itaendelea kuunga mkono juhudi za Mkoa wa Dodoma za kuboresha usafi wa mazingira. “Napenda kukupongeza Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa kwa juhudi zako za kuboresha mazingira ya Jiji la Dodoma ili livutie kwa usafi. Benki ya NMB tutakuwa nawe ili Dodoma iwe ya kijani” alisema Kimori.

Akiongelea zoezi la ugawaji wa vifaa vya kuhifadhia taka, alisema kuwa benki yake inatambua hitaji la vifaa vya kuhifadhia taka katika Jiji la Dodoma. Alisema kuwa idadi inayotakiwa ni vifaa 350 na kuahidi kuendelea kuunga mkono upatikanaji wake. “Rai yangu, tutumie na kutunza vifaa hivi ili kuliweka Jiji la Dodoma safi” alisema Kimori.

Kwa upande wa Naibu Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Emmanuel Chibago alisema kuwa vifaa hivyo ni muhimu kwa halmashauri. “NMB mmetusaidia Halmashauri ya Jiji la Dodoma kupunguza mzigo katika bajeti yetu. Tutavitunza vifaa hivi ili viwe endelevu” alisema Chibago.

Benki ya NMB ilikabidhi vifaa 100 vya kuhifadhia taka katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma vyenye thamani ya shilingi milioni 20 kwa lengo la kurahisisha zoezi la kuhifadhi taka katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.