• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma yadhamiria watoto wote wapate chakula shuleni

Imewekwa tarehe: March 1st, 2024

HALMASHAURI za Mkoa wa Dodoma zimetakiwa kuhakikisha zinafikia asilimia 80 ya shule zinazotoa chakula kwa wanafunzi wakati wa masomo. Hayo yameelezwa leo Februari pili, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule wakati wa kikao cha lishe cha robo ya pili ya mwaka (Oktoba - Desemba 2023) kilichofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Kikao hicho kimejikita kujadili umuhimu wa upatikanaji wa chakula shuleni pamoja na mikakati ya kuboresha huduma hiyo kwani chakula ni nguzo muhimu ya kusaidia kuinua taaluma na kutatua changamoto ya utoro hasa kipindi hiki ambacho Mkoa umeweka mkakati wa kuinua Elimu.

Senyamule amesema Mkoa umepiga hatua kwenye utekelezaji wa afua za lishe kwani lishe ndio jambo pekee lililosainiwa mikataba ya utekelezaji wake na Serikali.

"Mkoa wetu umeonesha matokeo mazuri kwa kipindi cha miezi 6 ya mwanzo wa mwaka 2023. Tumefikia 100.18% ya utekelezaji wa afua za lishe ambazo ni pamoja na 99.9% utoaji wa madini ya chuma kwa mama wajawazito, 100% matibabu ya utapiamlo, 101% unasihi kwenye ulishaji, 99.8% kwenye lishe, 105.3% utoaji wa vitamin A pamoja na 100% vikao vya lishe.

"Mpaka Sasa shule zinazotoa chakula ni 99% ingawa wanaotekeleza agizo hilo ni 64% tu. Tujiwekee mkakati angalau tufikie 75%. Viongozi muende mukalifanyie kazi kwa umakini kabisa hadi kufikia Juni 2024 tukamilishe. Mafanikio haya ni kutokana na ushirikiano wa Serikali na wadau hawa." Amesema Mhe. Senyamule.

Aidha, kikao hicho kimehudhuriwa na wadau mbalimbali wanaotekeleza miradi ya lishe kwenye Halmashauri za Mkoa wa Dodoma ambao ni Save the Children wanaotekeleza mradi wa 'Lishe yangu, maisha yangu', World Vision Tanzania, USAID, Sanku, Action against Hunger pamoja na Cuham ambapo miradi yao inajikita katika kupunguza utapiamlo kwa kusaidia upatikanaji wa chakula cha kutosha.

Hata hivyo, wakati wa kikao hicho, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dr. Bestie Magoma, ametumia kikao hicho kutoa taarifa ya maandalizi ya kampeni ya kitaifa ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa Surua itakayoanza Februari 15 hadi 18, 2024 ambapo maandalizi ya awali yanaendelea.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.