• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma yapongezwa kwa miundombinu ya barabara

Imewekwa tarehe: July 28th, 2021

WILAYA ya Dodoma imepongezwa kwa kupiga hatua kimaendeleo kufuatia ujenzi wa miundombinu inayoboresha maisha ya wananchi na huduma bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Kiongozi wa mbio za Mwenge maalum wa Uhuru kitaifa, Lt. Josephine Mwambashi alipokuwa akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kuulaki Mwenge Maalum wa Uhuru ulipoenda kuzindua barabara ya lami ya Kikuyu-Chidachi-Kinyambwa-Itega yenye urefu wa kilometa 6.05.

Lt. Mwambashi alisema kuwa ujenzi wa miundombinu ya barabara unalenga kuwezesha kupata huduma muhimu kwa haraka. “Barabara hii ni muhimu kwa sababu imesaidia kupunguza tatizo la kujaa maji katika eneo la shule na maeneo mengine kutokana na ujenzi wake na mifereji. Dodoma inaendelea sana, tofauti na miaka ya nyuma” alisema Lt. Mwambashi.

Aidha, aliwataka wafanyabiashara pembezoni mwa barabara kufanya usafi ili kutunza miundombinu hiyo na mazingira.

Baada ya kutembelea na kukagua barabara hiyo kisha kukagua na kujiridhisha na nyaraka, Kiongozi wa mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru alizindua barabara hiyo.  

Awali akisoma taarifa ya ujenzi wa barabara ya Kikuyu-Chidachi-Kinyambwa-Itega, Mratibu wa Mradi wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mhandisi Emmanuel Manyanga alisema kuwa lengo la ujenzi wa barabara hiyo lilikuwa kuboresha miundombinu ya mji. Lengo lingine ni kuwezesha mawasiliano baina ya wakazi wa eneo moja na lingine.

Kuhusu gharama za mradi huo, alisema kuwa asilimia 98.59 ililipwa. “Mpaka kufikia mwisho wa utekelezaji, Mkandarasi M/S Stecol Corporation kutoka China alilipwa shilingi 9,280,998,492.73 sawa ma asilimia 98.59 ya bajeti iliyotengwa” alisema Mhandisi Manyanga.

Mradi wa barabara hiyo ni sehemu ya Mradi wa Uendelezaji Miji ya Kimkakati (TSCP) uliofadhiliwa na Serikali kuu kupitia mkopo wa Benki ya Dunia.

Mwenge maalum wa Uhuru mwaka 2021 unaongozwa na kaulimbiu isemayo “TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu; itumie kwa usahihi na uwajibikaji”

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.