• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Dodoma yazindua Mkakati wa kutokomeza mbu na wadudu wadhulifu

Imewekwa tarehe: September 21st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge leo amezindua rasmi Mkakati wa kutokomeza mbu na wadudu wadhulifu katika mkoa wa Dodoma na kusisitiza kuwa mafanikio ya kiuchumi wa nchi yetu yanategemea sana wananchi kuwa na afya bora kwa kuepukana na maradhi.

Dkt. Mahenge ameyasema hayo leo kwenye uzinduzi huo wa kimkoa uliofanyika Jijini Dodoma, kata ya Mnadani kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Mnadani mbele ya mkutano mkubwa wa wananchi waliojitokeza tangu mapema asubuhi saa 12:30 ambapo shughuli hii ilianza kwa kufanya usafi eneo lote la shule ya Mnadani na mitaa inayozunguka shule hiyo.

Wakati tunapata Uhuru, Mwalimu Nyerere aliwatangaza maadui wakubwa wa nchi hii kuwa ni Ujinga, Umaskini na Maradhi, hata leo bado tunapambana na adui maradhi. Aliongeza kuwa Tanzania hatuwezi kujenga uchumi imara wa nchi yetu kama tunatendelea kuwa na changamoto ya maradhi kwa wananchi wetu. Alisema Mkuu wa Mkoa.

Kwa misingi hii, Rais wetu Dkt. John Magufuli wakati akiomba kula mwaka 2015 aliliona hili na kusisitiza kuwa endapo wananchi wanampa ridhaa ya kuiongoza nchi yetu, miongoni mwa mambo atakayoyashughulikia na kuyapa kipaumbele ni kujenga miundombinu ya huduma za Afya na kuongeza bajeti ya dawa na vifaa tiba. Akifafanua zaidi Dkt. Mahenge alisema kuwa, katika Mkoa wa Dodoma Serikali imejenga vituo vya Afya 21, na serikali pia imeongeza bajeti ya Afya kutoka shilingi milioni 900 hadi kufikia bajeti ya shilingi bilioni 4 kwa mwaka. Pia katika kipindi cha miaka mitatu ambacho serikali imekaa madarakani, tayari Hospitali 3 za Wilaya zimeanza kujengwa katika Wilaya za Chemba, Bahi na Chamwino, lakini pia Mhe. Rais aliamuru kujengwa kwa Hospitali ya Uhuru katika mkoa wa Dodoma kwa kutumia fedha ambazo zingetumika kugharamia sherehe za maadhimisho ya Uhuru.

Mahenge akakumbusha juu ya jitihada mbalimbali ambazo zimekuwa zikifanya na serikali kwa kuanzisha kampeni za kupambana na maradhi kama vile kampeni ya Jitambue, kampeni ya kupambana na maambukizi ya UKIMWI/VVU, kampeni ya kupambana na Maralia, kampeni ya Lishe na kadharika. Zote zikilenga kuimarisha afya za wananchi kwa ajili ya ustawi na maendeleo yao na nchi kwa ujumla. Hivyo akasisitiza kuwa kila mwananchi wa Dodoma pamoja na zoezi la kupiga dawa ya kuua mbu na wadudu wadhulifu, ni lazima kuhakikisha kila mmoja anafanya usafi nyumbani kwake, barabani na maeneo ya biashara ili kutokomeza uchafu na mazalia ya mbu kwenye maeneo yetu yanayotuzunguka kiasi cha mita tano.

Aidha, Mkuu wa Mkoa alilipongeza Jiji la Dodoma na Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma kwa kufanya maandalizi ya uzinduzi wa mkakati wa kutokomeza mbu na wadudu wadhulifu mkoani Dodoma. Katika kusisitiza na kuwaelekeza watendaji wa Wilaya kutekeleza hili, Dkt. Mahenge aliwagawia Wakuu wa Wilaya wote wa Wilaya za Mkoa wa Dodoma kitabu chenye mkakati wa kutokomeza mbu na wadudu wadhulifu ili wakasimamie mkakati huo katika maeneo yao ya kazi. Waliopewa ni wakuu wa Wilaya za Dodoma Mjini, Mpwapwa, Kongwa, Chamwino, Chemba, Kondoa na Bahi.


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.