• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Majaliwa: utekelezaji wa mipango ya kilimo upewe kipaumbele

Imewekwa tarehe: March 2nd, 2022

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango ihakikishe inaweka kipaumbele cha utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (DADPs) ikiwa ni pamoja na kutafuta fedha zitakazowezesha utekelezaji wake.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Machi 2, 2022) wakati akizindua Mipango ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (DADPs) katika ukumbi wa Chuo cha Mipango, jijini Dodoma. Pia amezitaka taasisi za fedha zijipange kutambua hati miliki za ardhi za wakulima kama dhamana ya kupata mikopo.

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezielekeza Halmashauri zote nchini zihakikishe zinatenga fedha kutoka katika mapato yake ya ndani kwa ajili ya utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ya Wilaya.

“Kwa kuwa asilimia kubwa ya rasilimali za utekelezaji wa ASDP II zinalenga kuelekezwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa, Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa waongeze usimamizi wa fedha na rasilimali.”

Waziri Mkuu amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa na Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wahakikishe wanawajenga uwezo wa kusimamia utekelezaji wa miradi katika ngazi mbalimbali na kubuni vyanzo vingine vya kupata fedha za kuendeleza miradi ya kuendeleza kilimo.

Mheshimiwa Majaliwa ameiagiza Ofisi ya Rais - TAMISEMI kupitia Halmashauri zote nchini ziendelee kutenga maeneo ili kuwawezesha wananchi kufanya shughuli za kilimo na shughuli nyingine kama vile ufugaji.

“Ofisi ya Rais TAMISEMI na Wizara ya Kilimo ziandae na kusimamia utekelezaji wa mkakati madhubuti wa kusimamia utendaji kazi wa maafisa ugani ili kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo. Maafisa Ugani wasimamiwe kikamilifu ili kuimarisha huduma za ugani kwa wakulima.”

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Innocent Bashungwa amesema watashirikiana na Wizara za Sekta ya Kilimo kutekeleza Mipango ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya kwa kutafuta rasilimali fedha na kusimamia kikamilifu matumizi na utekelezaji wake pamoja na kuimarisha mifumo ya kiteknolojia ya habari na mawasiliano katika sekta ya kilimo (TEHAMA) na kuwezesha upatikanaji wa huduma za kifedha.



Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.