• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Uwanja wa ndege Msalato, barabara ya Pangani mambo safi

Imewekwa tarehe: March 14th, 2020

SERIKALI ya Tanzania imepata mkopo wa masharti nafuu kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) wa Sh trilioni 1.14 kwa ajili ya kutekeleza miradi mitatu ya maendeleo.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato jijini Dodoma na ujenzi wa Daraja kwenye Kivuko cha Mto Pangani.

Hayo yamebainika jana jijini Dar es Salaam wakati wa kutiwa saini kwa mikataba hiyo, kulikofanywa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James na Mwakilishi Mkazi wa AfDB nchini, Dk Alex Mubiru.

Akizungumza baada ya kusaini mikataba hiyo, James alisema fedha hizo Shilingi trilioni 1.14 ni sawa na Dola za Marekani milioni 495.59, ambazo zimegawanywa kwenye miradi mitatu.

Alitaka miradi hiyo na kiasi cha fedha kitakachotumika kuwa ni Dola za Marekani milioni 271.63 zitatumika kwenye utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato, Dodoma, ambapo maandalizi ya mradi huo yameanza.

Akizungumzia mradi huo, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads), Patrick Mfugale alisema katika fedha hizo za AfDB, Dola za Marekani milioni 271.63 zimetengwa kuufanikisha ambazo ni sawa na Shilingi bilioni 757.78, huku pia serikali ikichangia fedha za ndani Sh bilioni 133.03 sawa na asilimia 17 ya fedha zote.

Mfugale alisema mradi huo wa ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Msalato utakaohudumia watu milioni 1.5, utahusisha barabara za kukimbilia ndege na ujenzi wa majengo ya abiria ya kisasa.

“Uwanja wa Msalato utakuwa uwanja wa kisasa mkubwa, wenye uwezo wa kuhudumia watu milioni 1.5 kwa wakati mmoja, uwanja utakuwa na urefu wa Kilomita 3.6 utakuwa na uwezo wa kuhudumia ndege aina ya Boeing 787 Dreamliner 17 na Airbus 380 kwa wakati mmoja,”alisema Mfugale.

Alisema hivi sasa mchakato wa kumpata mkandarasi umeshaanza, kwani zabuni ilifunguliwa Februari 13 mwaka huu na itafungwa Aprili 19, mwaka huu. Kwamba katika kutekeleza mradi huo, Sh bilioni 15.42 zimetengwa kwa ajili ya kuwalipa fidia wale watakaopaswa kuondoka kupisha mradi.

Kuhusu mradi wa pili utakaonufaika na fedha hizo za AfDB, James alisema ni Mradi wa Ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo- Horohoro/Lungalunga-Malindi na Ujenzi wa Daraja kwenye Mto Pangani, mradi unaotekelezwa kwa kiwango cha lami.

Mradi huo umetengewa Dola za Marekani milioni 168.76, ambazo ni sawa na Shilingi bilioni 448.6, huku huku pia serikali ikichangia Sh bilioni 58.473 sawa na asilimia 13.33 ya fedha zote .

Akifafanua mradi huo, Mfugale alisema katika utekelezaji wa mradi huo wa ujenzi wa barabara na daraja hilo, fidia ya Sh bilioni 10.3 imetengwa kwa watakaopaswa kuondoka, kupisha ujenzi wa barabara hiyo.

Aidha, mradi wa tatu uliopata fedha za AfDB jana ni Programu ya Utawala Bora na Kuendeleza Sekta Binafsi, ambapo umetengewa Dola za Marekani Milioni 55.2 Mwakilishi Mkazi wa AfDB nchini, Dk Alex Mubiru alisema fedha hizo zitasaidia kuimarisha maisha ya watu, kwa kuhakikisha miradi ya maendeleo itatekelezwa kwa ufanisi na kuleta tija kwa taifa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elius Mwakalinga alimshukuru Rais Johm Magufuli kwa kudumisha uhusiano nzuri baina ya wadau hao, ambao wamefanikisha utekelezaji wa miradi mingi nchini, ambayo hadi sasa inafikia Dola za Marekani bilioni 2.1.

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Doto James (kushoto), akisaini Mikataba mitano yenye thamani ya Dola za Marekani 495.59 na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Alex Mubiru (kulia) katika hafla iliyofanyika Benki Kuu Jijini Dar es Salaam.

Afisa Mtendaji Mkuu Tanroad, Patrick Mfugale akizungumza katika hafla ya utiaji saini wa mikataba ya Ujenzi wa Kiwanja cha Ndege wa Kimaifa wa Msalato Jijini Dodoma, Ujenzi wa Barabara ya Bagamoyo-Pangani-Tanga uliofanyika katika Ukumbi wa Benki Kuu ya Tanzania, Jijini Dar es Salaam.


Chanzo: habarileo.co.tz

Tazama pia:- AfDB imeipatia Tanzania Mkopo wa Masharti Nafuu US Dola Milioni 495.59 

                  -  Benki ya Maendeleo ya Afrika - AfDB yaahidi kuipatia Tanzania mikopo nafuu kutekeleza miradi ya maendeleo

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.