• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Elimu bure yaanza kutoa matunda, wadau wajitokeza

Imewekwa tarehe: January 14th, 2020

TAASISI mbalimbali na watu binafsi, wameonesha nia ya kumsaidia mwanafunzi, Yonana Lugedenga pamoja na familia yake, kumwezesha aendelee na masomo yake, baada ya kufaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza, licha ya mazingira magumu aliyosomea.

Aidha, upande wa serikali, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anthony Mtaka amesema mwanafunzi huyo ambaye ni tunda la mafanikio ya sera ya elimu bure, atapewa Sh milioni moja na kununuliwa vifaa vinavyohitajika, kujiunga na kidato cha tano, kama ilivyo kwenye mpango uliofikiwa na mkoa. Hata hivyo, Mtaka alisema jana kutokana na maoni na hoja mbalimbali, zilizotolewa kuhusu mwanafunzi huyo, katika tathimini watakayoifanya, wataangalia uwezekano wa kuweka pia mpango wa kufuatilia na kuwezesha wanafunzi wanaofaulu hadi chuo kikuu.

Yohana ambaye amehitimu Shule ya Sekondari ya Igaganulwa Kata ya Dutwa wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, amefaulu mtihani wa kidato cha nne kwa kupata alama A masomo yote tisa. Mtaka alisema miongoni mwa taasisi ambazo zimewasiliana naye, zikitaka kumsaidia mtoto huyo ni Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), lililosema linataka kumsaidia.

“Unesco wamenipigia simu, nadhani wanataka kum-support. Wana nia hata ya kusaidia wadogo zake…” alisema na kuongeza kuwa pia mkurugenzi mtendaji wa benki ya NMB na watu binafsi, waliowasiliana naye, walionesha kuwa wana jambo wanataka kulifanya.

Akizungumzia matokeo na mjadala ulioibuka, kuhusu ufaulu wa Yohana aliyekuwa akisoma shule ya kata ya Igaganulwa, Mtaka alisema ni uthibitisho wa umma, kuanza kuamini shule za serikali.

Alisema jambo ambalo umma haujafahamishwa ni kwamba mwanafunzi huyo, anamulika mafanikio ya sera ya elimu bure, iliyoanza kutekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk John Magufuli.

“Hii ndiyo Form Four (kidato cha nne) ya kwanza tangu Rais Magufuli aingie madarakani. Kama isingekuwa elimu bure huyu mtoto angewezaje kusoma? Maeneo kama haya (vijijini) maisha yalikuwa magumu. Hata huyu mtoto asingeweza kusoma,” alisema Mtaka.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga akimzungumzia kijana huyo alisema “Inatia hamasa sana na kumshukuru sana Rais wa Awamu ya Tano, Dkt. John Magufuli kwa kuleta elimu bure. Maana taarifa ni kwamba kijana huyu hata uniform (sare) za shule kwa miaka yote alikuwa ananunuliwa na walimu wake kwa vile alijulikana kwa kuwa na akili nyingi sana”.

Kulingana na mkakati wa mkoa, kuhusu watoto wa shule za serikali wanaofaulu kwa kupata alama 7 kwa maana ya A katika masomo yote kidato cha nne, hupewa Sh milioni moja za kukidhi mahitaji yake. Vivyo hivyo, kwa kidato cha sita kwa mwenye ufaulu wa alama 3.

Kwa mujibu wa Mtaka, mwaka jana pia mkoa wa Simiyu ulipata mwanafunzi aliyefaulu kwa alama 7 kutoka shule ya serikali. Alitoka Shule ya Sekondari ya kata ya Nkololo wilayani Bariadi. Akizungumzia kambi za kitaaluma, Mkuu wa Mkoa alisema zimekuwa na faida kubwa.

Alisema mwaka 2016 alipofika Simiyu, katika mitihani yote ya kitaifa; darasa la nne, la saba, kidato cha pili, cha nne na sita, mkoa ulikuwa ukishika nafasi za 26,25 na 22.

“Lakini leo katika mitihani yote, mkoa umeingia kumi bora. Utaona mwaka 2016 katika kidato cha nne tulikuwa wa 22, mwaka 2017 wa 14, mwaka 2018 wa tisa na mwaka 2019 tukawa wa tano. Wakati huo huo katika Darasala la Saba mwaka 2018 tulikuwa wa 22, mwaka 2019 namba tisa,” alisema Mtaka.

Kwa mujibu wa Mtaka, mwaka jana, katika matokeo kwa shule za serikali, Simiyu iliingiza watoto wanne katika 10 bora na shule moja katika shule 10 bora. Mtaka alisema jambo ambalo linapaswa kuzingatiwa na serikali ni kutafuta namna ya kusaidia watoto, kuondokana na kusafiri umbali mrefu kwenda shule.

Chanzo: habarileo.go.tz


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.