• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Elimu ni haki ya watoto wenye mahitaji maalum Kata ya Ipagala

Imewekwa tarehe: January 11th, 2025

Na. Coletha Charles, IPAGALA

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imeendelea na jitihada ya utambuzi wa watoto wenye mahitaji maalum kiafya kwa lengo la kujiunga na elimu ya awali na msingi kwa mwaka wa masomo 2025 katika Kata ya Ipagala.

Akizungumza wakati zoezi hilo, Afisa Elimu wa Kata ya Ipagala, Veronica Mpanda, aliwaomba wazazi kuwapeleka watoto wenye mahitaji maalum shule kwa sababu wanahaki ya kupata elimu kama watoto wengine kulingana na sera ya elimu jumuishi kwa kuwa miundombinu imara ipo kwa ajili yao.

Alisema kuwa zoezi hilo linalenga kutambua idadi na aina ya mahitaji ya watoto hao ili kuweka mipango madhubuti ya kuwahudumia. “Zoezi hili la uandikishaji lilitakiwa lifanyike katika Shule ya Msingi ya Ipagala B, lakini hatujafanikiwa kupata mtoto hata mmoja mwenye mahitaji maalum japo zoezi hili ni endelevu na tunatambua kwamba elimu ni haki ya kila mtoto na kupitia zoezi hili tutahakikisha kuwa hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa sababu ya changamoto yoyote” alisema Mpanda.

Nae, Msimamizi Msaidizi wa Kituo cha Upimaji Shule ya Msingi Nkuhungu, Deogratias Montano, alisema kuwa wanawapima na kuwapangia watoto hao shule stahiki ambazo wanaweza kusoma bila shida na zoezi hilo litaendelea ndani ya wiki mbili.

Alisema kuwa mwitikio bado siyo mzuri kwa wazazi na walezi wa watoto wenye mahitaji maalum japokuwa wamejipanga kutokuacha mtoto nyumbani ambaye ana ulemavu wa macho, ulemavu wa viungo, mtindio wa ubongo na ulemavu wowote. “Tunashirikiana kwa karibu na wazazi na walezi wa watoto hawa ili kuhakikisha tunapata taarifa sahihi. Hii inatusaidia kupanga huduma zinazofaa kulingana na mahitaji ya kila mtoto na hatua hii ni muhimu kwa maendeleo ya jamii nzima. Elimu inatakiwa itolewe kwa upana juu ya jamii kuhusu umuhimu wa kuwasaidia watoto” alisema Montano.

Halmashauri ya Jiji la Dodoma imejipanga kuboresha hali ya watoto wenye mahitaji maalum kwa kuhakikisha wanajumuishwa kikamilifu katika mfumo wa elimu na maisha ya kila siku.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.