• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

EWURA yatangaza bei kikomo Petroli, Dizeli

Imewekwa tarehe: September 4th, 2020

MAMLAKA ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya petroli nchini.

Kwa mujibu wa EWURA, mwezi huu bei hizo zimeongezeka, ikilinganishwa na mwezi uliopita.

Taarifa ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo, Godfrey Chibulunje imebainisha kuwa bei hizo mpya, zitaanza kutumika kuanzia leo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kwa Septemba bei za rejareja za petroli, dizeli na mafuta ya taa, zimeongezeka kwa Sh 20 kwa lita (sawa na asilimia 1.11), Sh nane kwa lita (sawa na asilimia 0.46) na Sh 124 kwa lita (sawa na asilimia 7.93).

“Ikilinganishwa na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za petroli, dizeli na mafuta ya taa zimeongezeka kwa shilingi 20.19 kwa lita (sawa na asilimia 1.18), shilingi 8.14/lita (sawa na asilimia 0.49) na shilingi 123.89/lita (sawa na asilimia 8.58),”ilieleza taarifa hiyo iliyotolewa jana.

Ilieleza kuwa mwezi huu bei za jumla na rejareja kwa mafuta ya petroli na dizeli kwa Mikoa ya Kaskazini (Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara) zimepungua ikilinganisha na bei zilizotolewa mwezi uliopita.

Taarifa ilieleza kuwa bei hizo zimepungua kwa petroli na dizeli kwa Sh 19 kwa lita (sawa na asilimia 1.04) na Sh tano kwa lita (sawa na asilimia 0.25), mtawalia.  

Vilevile, ilieleza kuwa ukilinganisha na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za Petroli na Dizeli zimepungua kwa Sh 19.35 kwa lita (sawa na asilimia 1.11) na Sh 4.51 kwa lita (sawa na asilimia 0.27), mtawalia.

Taarifa ya Chibulunje ilieleza kuwa bei za mafuta ya taa hazina mabadiliko na zitaendelea kuwa zile zilizotangazwa katika toleo lililopita la Agosti 5, mwaka huu.

“Hii ni kwa sababu, kwa mwezi Agosti hakuna shehena ya mafuta iliyopokelewa nchini kupitia bandari ya Tanga,” ilieleza taarifa hiyo.

Taarifa ilieleza kuwa, mwezi huu bei za rejareja na jumla kwa bidhaa za mafuta ya Petroli na Dizeli kwa Mikoa ya Kusini (Mtwara, Lindi, and Ruvuma) zimeongezeka ikilinganisha na bei zilizotolewa mwezi uliopita.

Ilibainisha kuwa mwezi huu, bei hizo za rejareja za Petroli na Dizeli zimeongezeka kwa Sh 11 kwa lita (sawa na asilimia 0.60) na Sh 16 kwa lita (sawa na asilimia 0.91), mtawalia.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo vilevile, ukilinganisha na toleo la mwezi uliopita, bei za jumla za Petroli na Dizeli zimeongezeka kwa Sh 11.19 kwa lita (sawa na asilimia 0.64) na Sh 16.36/lita (sawa na asilimia 0.98).

Alisema mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la ndani, yanatokana na mabadiliko ya bei za mafuta katika soko la dunia, gharama za usafirishaji na gharama za ucheleweshaji wa ushushaji wa mafuta.

“Ewura inapenda kuukumbusha umma kwamba bei kikomo za mafuta kwa eneo husika zinapatikana pia kupitia simu za mkononi kwa kupiga namba *152*00# na kisha kufuata maelekezo. Huduma hii ni bure na inapatikana kupitia mitandao yote ya simu za mkononi hapa nchini,” ilieleza taarifa hiyo.

Ilieleza kuwa kwa mujibu wa Sheria ya Mafuta ya mwaka 2015, bei za bidhaa za mafuta ya petrol, zitaendelea kupangwa na soko.

“EWURA itaendelea kuhamasisha ushindani kwa kutoa taarifa za bei kikomo za bidhaa za mafuta. Taarifa hizi zina lengo la kuwasaidia wadau kufanya maamuzi stahiki kuhusu manunuzi ya bidhaa za mafuta,”ilieleza taarifa hiyo.

Taarifa ya Chibulunje ilisisitiza kuwa kampuni za mafuta ziko huru kuuza bidhaa za mafuta ya petroli kwa bei ya ushindani, ilimradi tu bei hizo zisivuke bei kikomo (kama ilivyokokotolewa na kanuni iliyopitishwa na Ewura na ambayo ilichapishwa katika Gazeti la Serikali Namba 74 la Februari mwaka huu).

“Vituo vyote vya mafuta vinatakiwa kuchapisha bei za bidhaa za mafuta katika mabango yanayoonekana bayana na yakionesha bei ya mafuta, punguzo, vivutio vya biashara au promosheni zinazotolewa na kituo husika,” ilielekeza taarifa hiyo.

Chanzo: HabariLeo





Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.