• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Fadhili Chibago, Naibu Meya Jiji la Dodoma

Imewekwa tarehe: August 15th, 2024

Na; Francisca Mselemo

MKUTANO wa mwaka wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma umefanyika Leo Agosti 15,2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Jiji, ukiwa na ajenda muhimu za kujadili  mipango iliyotekelezwa na  matumizi yaliyofanyika katika mwaka wa fedha uliopita, yaani 2023/2024,  pamoja na uchaguzi wa Naibu Meya, wenyeviti,na wajumbe wa kamati za kudumu za Halmashauri.

Katika mkutano huu, Madiwani walijadili masuala mbalimbali yanayohusiana na utendaji, ikiwa ni pamoja na huduma za Afya na ukusanyaji wa mapato. Moja ya matukio muhimu katika mkutano huo, ilikuwa ni uchaguzi wa Naibu Meya,huku Mgombea katika uchaguzi, akiwa mmoja tu ambaye ni mheshimiwa Fadhili Chibago,diwani wa  kata ya Dodoma Makulu.

Kwa mujibu wa kanuni,Wajumbe walitakiwa kupiga kura za ndiyo au hapana,ndipo zoezi la kupiga kura lilipofanyika, kura zilizopigwa zilikuwa 47, kura moja iliharibika,kura 46 zilikuwa za ndiyo,hatimaye, baada ya mchakato wa uchaguzi, Naibu Meya mpya alipatikana, akitarajiwa kuimarisha ushirikiano kati ya Madiwani na Menejimenti  ya Jiji.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo yaliyompa ushindi,Naibu Meya huyo mpya alikuwa na haya ya kusema,

“ Nawashukuru sana kwa kunichagua kwa kura nyingi,nashukuru sana kwa heshima mliyonipa,na imani kubwa  mliyoionyesha kwangu.Lakini Mimi bila ninyi,siwezi,nawategemea sana tushirikiane katika kila jambo,mnishauri,na mnionye pia pale nitakapokosea.Nawashukuru sana,na nawaahidi utumishi makini sana,utumishi bora”.

 Aidha,mkutano huo pia ulijumuisha uchaguzi wa wajumbe na wenyeviti wa kamati za kudumu za Halmashauri. Kamati hizo zina jukumu muhimu la kusimamia shughuli mbalimbali za Halmashauri na kuhakikisha kwamba Wananchi wanapata huduma bora,na mipango ya maendeleo inatekelezwa kwa ufanisi.Wajumbe walichaguliwa kwa kuzingatia ujuzi wao, uzoefu, na uwezo wa kushirikiana na Wananchi katika kutatua changamoto zinazowakabili.

Katika hatua nyingine, mkuu wa idara ya Mipango na uratibu wa Jiji,ndugu Francis Kaunda aliwasilisha taarifa ya Kiutendaji ya mwaka iliyojumuisha,mapato na matumizi.

“Katika mwaka wa fedha 2023/2024 Halmashauri ya jiji la Dodoma ilipanga kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 123.8,ilifanikiwa kutumia bilioni 131.Sisi Halmashauri ya Jiji la Dodoma,tunamshukuru sana  Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Daktari Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi.Fedha ambazo hazikuwa kwenye bajeti ya Halmashauri,lakini zimesababisha utekelezaji wa miradi mikubwa’’.Alisema Kaunda.

 Kwa ujumla, mkutano wa mwaka wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Dodoma ulikuwa na mafanikio, ukionyesha dhamira ya Madiwani katika kuboresha Huduma za Jamii na maendeleo ya Jiji. Hali hii inatoa matumaini makubwa kwa wananchi wa Dodoma wanaotarajia kuona mabadiliko chanya kupitia Uongozi mpya.




Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.