• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Fountain Gate wapongezwa kwa kuibuka mabingwa mashindano ya CECAFA

Imewekwa tarehe: February 23rd, 2023

Na. Mwandishi Maalum, DODOMA

TIMU ya wasichana ya mpira wa miguu ya Fountain gate imepongezwa kwa kuibuka bingwa wa mashindano ya shule za sekondari za Academy yaliyoandaliwa na CAF Africa ukanda wa CECAFA na kuichora ramani ya Jiji la Dodoma kwenye mpira.

Pongezi hizo zilitolewa na Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe katika hafla kabambe ya kuipokea na kuipongeza timu ya wasichana ya mpira wa miguu ya Fountain gate katika ukumbi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma.

Prof. Mwamfupe alisema kuwa timu hiyo ya wasichana imeichora ramani ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwenye mpira. “Hakuna Mstahiki Meya yeyote katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati wakati huu anayeongea na mabibwa wa CECAFA isipokuwa Meya wa Jiji la Dodoma. Hivyo, Halmashauri ya Jiji la Dodoma tumekuwa kinara kwenye mambo mengi sana, lakini mabinti hawa wa Fountain gate mmetung’arisha zaidi” alisema Prof. Mwamfupe.

Aidha, Mstahiki Meya huyo alishauri kuwa liandaliwe bango kubwa la chuma lenye majina na picha za wasichana hao mabingwa wa CECAFA katika shule ya sekondari ya Fountain gate ili iwe kumbukumbu kwao na vizazi vijavyo.

Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Mwalimu Upendo Rweyemamu alisema kuwa wanafunzi wa kike wa shule ya sekondari Fountain gate wameipa heshima Halmashauri ya Jiji la Dodoma na taifa kwa ujumla. “Mabinti wa Fountain gate wameleta heshima kwa Mkoa wa Dodoma, wameleta heshima kwa Jiji la Dodoma, wameleta heshima kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kuchukua ubingwa wa CECAFA” alisema Rweyemamu.

Alisema kuwa Halmashauri ya Jiji inajivunia mabinti hao kwa kudhihirisha umuhimu wa michezo kwa wanafunzi. “Mheshimiwa mgeni rasmi, mabinti hawa wanafanya vizuri katika taaluma. Hakika wamedhihirisha kuwa taaluma na michezo vinakwenda pamoja. Hapa tunazungumza na mabinti wanaokwenda Afrika ya Kusini kutetea ubingwa wa CECAFA” alisema Mwalimu Rweyemamu wakati akitabasamu.

Aidha, aliwataarifu kuwa michezo ni ajira. Kupitia michezo alisema kuwa wamekuza uchumi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma na Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.

Mashindano ya CECAFA kwa shule za sekondari yalianza tarehe 16-19 Februari, 2023 jijini Dar es Salaam na timu ya wasichana ya Fountain gate ya jijini Dodoma iliibuka kidedea ikiwa na wachezaji 15 na walimu wa nane ilitunukiwa dola za kimarekani 100,000.

MWISHO

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.