• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Wananchi watakiwa kufuata utaratibu kabla ya kuanza ujenzi

Imewekwa tarehe: July 27th, 2020

WAKAZI wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma wametakiwa kufuata sheria zilizopo kabla ya kuanza ujenzi ili kuepuka kujenga kinyume na taratibu za mipango miji nchini na kulifanya Jiji hilo kujengeka kiholela.

Rai hiyo ilitolewa na kiongozi wa timu namba moja ya wajumbe wa menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alipokuwa akiongelea utekelezaji wa zoezi hiko lililoanza mapema asubuhi jijini hapo leo.

Kimaro ambaye pia ni mkuu wa idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu alisema kuwa kumekuwepo na tabia inayoendelea kukua ya kujenga bila kuwa na vibali vya ujenzi. “Tumefanya ziara ya ukaguzi wa maeneo mbalimbali ambayo ujenzi unaendelea. Hii ni baada ya Halmashauri ya Jiji kubaini watu wengi wanafanya uendelezaji na ujenzi ambao hauna vibali na kutozingatia taratibu za uendelezaji wa mji. Tulichobaini katika timu yetu, watu wengi wanafanya ujenzi bila kuwa na vibali vya ujenzi. Na kwa kweli tumewasimamisha wasiendelee na ujenzi mpaka watakapopata vibali halali vya ujenzi” alisema Kimaro.

“Katika ukaguzi huu tumebaini mambo ya ajabu sana. Unakuta maeneo ya makazi yaliyopimwa lakini kuna biashara ambazo zimeanzishwa za kufyatua tofali kinyume ya masharti ya kibali na matumizi ya eneo husika” alisema Kimaro.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi wa Dodoma, kuhakikisha kabla ya kuanza ujenzi wanafuata taratibu zote za mipango miji ambazo ni kuwa na ramani zilizopitishwa na mamlaka husika, kuwa na vibali sahihi vya ujenzi ambavyo vimepitishwa na mamlaka na Jiji, na kujiepusha na ujenzi holela usiofuata taratibu. “Kukiuta kufuata utaratibu kutasabisha kuvunjiwa majengo hayo. Wananchi wote wanatakiwa kutii sheria bila shuruti” alisisitiza Kimaro.

Kwa upande wa fundi sanifu ujenzi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Issac Emmanuel alisema kuwa changamoto kuwa ni maeneo yaliyopimwa watu wanajenga tofauti ya masharti ya vibali vyao vya ujenzi.

“Yapo maeneo ambayo yamepimwa, unakuta mtu kapewa kibali cha ujenzi wa nyumba moja ila anajenga ‘two in one’. Maeneo mbayo yamepangwa kwa makazi tu, unakuta mtu kajenga fremu za biashara. Maeneo yametengwa kwa ajili ya makazi, mtu anajenga taasisi bila kuwa na kibali chochote. Unakuta watu wengine wanaendelea na ujenzi wakati vibali vyao havijapitishwa na Halmashauri” alisema Emmanuel kwa masikitiko.

Timu ya menejimenti ya Halmashauri ya Jiji la Dodoma ilijigawa katika makundi manne, na kundi hili kutembelea maeneo ya Itega, Kinyambwa na Kikuyu kukagua ujenzi usiozingatia taratibu.

Mwenyekiti wa Kundi Na. 1 la Timu ya Menejimenti ya Jiji la Dodoma Dickson Kimaro (kulia) akiwa na maafisa wengine wa Jiji la Dodoma Omari Mafia (kushoto) na Isaya Kimei (kushoto kwa Mafita) wakikagua vibali vya ujenzi kutoka kwa msimamizi wa ujenzi wa moja ya maeneo waliyotembelea kubaini wanaojenga bila kufuata taratibu halali za ujenzi.


Baadhi ya maeneo yaliyokutwa ujenzi ukiendelea bila kufuata taratibu za ujenzi na kuzuiliwa kuendelea na ujenzi.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.