• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Government City Complex kulibeba Jiji kimapato - DC Shekimweli

Imewekwa tarehe: July 28th, 2021

MRADI wa ujenzi wa Government City Complex utaiwezesha Halmashauri ya Jiji la Dodoma kujitegemea kimapato baada ya kukamilika kwake.

Kauli hiyo ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alipokuwa akimshukuru Kiongozi wa mbio maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 baada ya kuweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi wa Government City Complex jijini Dodoma.

Shekimweri alisema “mradi huu utatufanya Halmashauri ya Jiji la Dodoma kuweza kujitegemea kimapato”. Sifa ya halmashauri yenye hadhi ya jiji ni uwezo wa kujitegea kimapato, aliongeza na kuutaja mradi huo kuwa umetafsiri maana ya serikali kuhamia Dodoma.

Akiongea na mamia ya wananchi waliojitokeza kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi mradi huo, Kiongozi wa mbio maalum za Mwenge wa Uhuru kitaifa, Lt. Josephine Mwambashi aliwataka wanaosimamia miradi ya serikali kuwa makini. “Lazima tuwe makini kusimamia miradi hii, ioneshe kuwa tupo na uzalendo usio na shaka. Niwatake kuzidisha ushirikiano kwenye utekelezaji na usimamizi wa miradi ya maendeleo” alisisitiza Lt. Mwambashi.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa ujenzi wa mradi wa Government City Complex kwa Kiongozi wa mbio hizo, Mkuu wa Idara ya Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji, Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Shaban Juma alisema kuwa lengo la mradi huo ni kuongeza mapato ya halmashauri na kutoa huduma kwa wananchi.

Akiongelea ujenzi wa mrahi huo, alisema kuwa utekelezaji wake ulianza tarehe 1 Septemba, 2019 na ulitarajiwa kukamilika tarehe 31 Disemba, 2020. “Hata hivyo mkandarasi aliongezewa muda hadi tarehe 31 Agosti, 2021. Mradi huu unatekelezwa na mkandarasi M/S Mohammed Builders Ltd. Chanzo cha fedha za mradi huu ni mapato ya ndani” alisema Juma.

Kuhusu matumizi ya TEHAMA, mkuu huyo wa idara alisema “majengo yatatumia mifumo mbalimbali ya TEHAMA kama vile mfumo wa ukusanyaji wa mapato, mfumo wa ulinzi kwa kutumia camera, mfumo wa ving’amuzi moto, mfumo wa kununua vyumba kwa mtandao na uwepo wa huduma za mtandao za bure.

Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 unaongozwa na kaulimbiu isemayo “TEHAMA ni msingi wa Taifa endelevu; itumie kwa usahihi na uwajibikaji”.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.