• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Hakuna sheria iliyowekwa kukandamiza wengine” RC. Senyamule

Imewekwa tarehe: February 9th, 2024

WITO umetolewa wa Maafisa usafirishaji wa Bajaji na Pikipiki (Bodaboda) Jijini Dodoma kufuata sheria za barabarani zilizowekwa na Mamlaka husika ili kuepuka kadhia wanazozipata pindi wanapokua kazini. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, alipokutana na kundi hilo kwenye ukumbi wa ofisi yake iliyopo jengo la Mkapa.

Mkuu wa Mkoa huyo, ameitisha kikao hicho ikiwa ni utaratibu wake wa kukutana na makundi mbalimbali ya kijamii yaliyopo ndani ya Mkoa wa Dodoma kusikiliza na kutatua kero zinazowakabili. Katika kikao hicho, kero kadhaa ziliwasilishwa na nyingi zikapatiwa ufumbuzi ikiwemo ya uvunjaji wa sheria za barabarani ambapo amewataka madereva hao kufuata sheria kwa ustawi wa Mkoa.

“Sheria hizi zimewekwa ili tuzifuate na hakuna sheria iliyowekwa kwa ajili ya kumkandamiza mwananchi. Lengo hasa ni kuimarisha ulinzi na usalama wa raia. Nyinyi ni viongozi, kaeni na wenzenu munapokua kwenye vituo vyenu, peaneni ushauri wa namna ya kujiendeleza kwenye mambo ya msingi.

“Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anathamini makundi yote ya kijamii yaliyopo katika maeneo yetu na yote anayapa uzito ulio sawa hivyo na sisi tunapaswa kufanya hivyo kwani Rais wetu anatamani kila mmoja awe na furaha.” Amesisitiza Mhe. Senyamule

Akijibu Baadhi ya kero zilizowasilishwa kwenye kikao hicho ambazo nyingi zililenga Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini LATRA inayojishughulisha na utoaji wa leseni za usafirishaji, Ezekiel Emmanuel ambaye ni Afisa Mfawidhi wa Mamlaka hiyo amesisitiza umuhimu wa kuwa na leseni ya usafirishaji ili kuepuka kadhia barabarani

“Mtu yeyote anayekusudia kufanya shughuli ya usafirishaji wa abiria, sharti nawe na leseni ya LATRA. Kinyume na hapo ni kosa la jinai na atapigwa faini ya shilingi 25,000. Tutii sheria bila shuruti kuepuka ukamataji holela. Tuhamasishane kwenye vituo vyetu kuepukana na haya. Tunatafuta riziki lakini sio kwa uvunjifu wa amani” Amesema Emmanuel.

Jiji la Dodoma lina takribani vituo vya Bajaji na Bodaboda 394 vilivyosajiliwa huku waendesha vyombo hivyo waliosajiliwa wakifikia takribani 400. Mkoa unathamini mchango wa sekta ya usafirishaji.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.