• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hakuna ugonjwa wa Ebola Tanzania - Waziri Ummy

Imewekwa tarehe: September 16th, 2019

Serikali imesema hakuna ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania na  kuwataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na kudhibiti ugonjwa huo usiingie nchini kutoka nchi  za jirani ikiwemo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (Congo DRC)

Hatua hiyo inakuja baada ya taarifa kuzagaa katika mitandao ya kijamii zikidai kuwa ugonjwa huo umeingia nchini na baadhi ya watu wameanza kufariki kwa Ebola.

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu aliyekuwa akitoa taarifa rasmi ya Serikali kuhusu ugonjwa huo Septemba 14, 2019 jijini Dar es Salaam amesema mpaka sasa hakuna mgonjwa yeyote aliyethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola.

"Wizara inawasihi wananchi, kutokuwa na hofu kwani mpaka sasa hivi hakuna mgonjwa yeyote ambaye amethibitishwa kuwa na ugonjwa wa Ebola nchini Tanzania,” amesema Mwalimu.

Hata hivyo, amewataka wananchi kuchukua tahadhari ya kujikinga na kudhibiti  ugonjwa huo ambao umeripotiwa katika nchi jirani usiingie nchini.

"Ikumbukwe kuwa ugonjwa wa Ebola umethibitika kuwepo nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambapo ilitolewa taarifa kwa mara ya kwanza Agosti 2018 na hadi kufikia Septemba 12, 2019,  kuna jumla ya wagonjwa 3,099 ambao wamethibitishwa kuwa na ugonjwa huo,” amesisitiza Mwalimu.

Amesema  wizara yake  inapenda kuwahakikishia Watanzania kuwa tangu ugonjwa huo uliporipotiwa katika nchi jirani imeweka mikakati na kuchukua hatua mbalimbali za kuhakikisha ugonjwa huo unadhibitiwa ili usiingie nchini kwa kufanya masuala mbalimbali ikiwemo kuimarisha ufuatiliaji wa ugonjwa huo kupitia katika wataalam wa afya katika mikoa, wilaya na maeneo ya mipakani.

Pia wizara imeimarisha uchunguzi wa wageni wanaoingia nchini kupitia mipakani na kununua vifaa mbalimbali ikiwemo kipima joto, ambavyo wasafiri kutoka nchi mbalimbali wanaohisiwa kuwa na ugonjwa huo wamekuwa wakipimwa kabla ya kuingia nchini.

Aidha, Serikali imenunua na kusambaza seti takriban 2,700 za mavazi kinga kwenye mikoa yote iliyo katika hatari ya kukumbwa na tishio la Ebola ambayo mikoa hii ni Kigoma, Kagera, Mwanza, Rukwa na Katavi, kwa sababu inapakana na DRC.

Dalili kuu za ugonjwa wa Ebola ni homa kali, kuumwa na kichwa, kutapika, kuharisha, viungo vya mwili kuuma, kutokwa na vipele mwilini na kutokwa na damu katika matundu ya mwili.

Chanzo:afyablog.moh.go.tz/


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.