• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Halmashauri mjipime, mjitathmini kwenye mapato - Mhe. Majaliwa

Imewekwa tarehe: July 24th, 2019

MAMLAKA za Serikali za Mitaa nchini zimetakiwa kujipima na kujitathmini katika ukusanyaji wa mapato kwa mujibu wa malengo ya ukusanyaji kodi.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa (Mb) alipokuwa akifungua mkutano mkuu wa 35 wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (ALAT) kwa niaba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli jijini Mwanza jana.

Majaliwa alisema Halmashauri zinatakiwa kujitathmini juu ya ukusanyaji wa mapato yao ya ndani kulingana na malengo waliyojiwekea.

“Kuna Halmashauri zimetajwa hapa kwamba hazijafikia malengo ya makusanyo ya ndani. Fanyeni tathmini, ni kwa nini hamjafikia malengo na mhakikishe kuwa mwakani hamji kutajwa tena kwenye mkutano kama huu”, alisema Majaliwa. Halmashauri hizo ni Kakonko, Buhigwe, Madaba, Kigoma, Momba na Songea.

Waziri mkuu aliwataka Meya, Wenyeviti wa Halmashauri na Wakurugenzi wa Mamkala za Serikali za mitaa kusimamia makusanyo na matumizi ya mapato ili yatumike katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo nchini.  Aidha, aliwataka kutenga asilimia 40 kwa ajili ya shughuli za maendeleo kutoka kwenye makusanyo ya ndani. Alisema kuwa dhamira ya serikali ni kuona Halmashauri zinajitegemea kwa asilimia 80-100 ifikapo mwaka 2025.

Akiongelea uamuzi wa serikali kukusanya fedha zote na kuziweka katika chanzo kimoja, alisema kuwa uamuzi huo ulitokana na utafiti wa muda mrefu uliobaini kuwa fedha zilizokuwa zinakusanywa zilikuwa haziendi kwenye miradi ya maendeleo inayowalenga moja kwa moja wananchi.

Awali Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa,  Mhe. Selemani Jafo (Mb) alisema kuwa serikali inajivunia ujenzi wa shule za sekondari za Kata. Alisema kuwa shule hizo zimefanya vizuri katika mtihani wa kumaliza kidato cha sita mwaka 2019. “Kati ya shule bora 100, shule 64 ni za Serikali na kazi ya shule hizo 64, shule 54 ni za kata. Na kwenye matokeo ya masomo ya sanaa, kati wanafuzi bora 10 wa kiume, wanafunzi saba wanatoka kwenye shule za kata,” alisema Jafo.

Waziri huyo aliipongeza Serikali kwa kutenga sh. bilioni 268.8 kwa ajili ya ujenzi wa miradi 38 ya kimkakati kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa ambayo ni ujenzi wa stendi za mabasi, masoko na machinjio.

Mkutano wa ALAT unafanyika jijini Mwanza kwa siku tatu ukihudhuriwa na washiriki zaidi ya 600 wakiwemo Mameya wa Majiji na Manispaa, Wenyeviti wa Halmashauri za Miji na Wilaya na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za mitaa.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akifurahia jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), katika mkutano mkuu wa 35 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT), uliyofanyika katika ukumbi wa Malaika, jijini Mwanza, Waziri Mkuu amemwakimwakilisha Rais Magufuli katika mkutano huo, Julai 23.2019.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Mstahiki Meya wa Jiji la Dodoma atoa pongezi kwa Madiwani

    May 25, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Mkopo wa 10% tija kwa maendeleo ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu

    May 23, 2025
  • Wananchi Kata ya Madukani washukuru kuboreshwa huduma za Afya, Zahanati ya Chikande

    May 21, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.