• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Halmashauri yaongeza uwezo kujitegemea, sasa 42%

Imewekwa tarehe: September 22nd, 2021

Na Sifa Stanley, DODOMA.

MSTAHIKI Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Prof. Davis Mwamfupe amesema kuwa halmashauri hiyo inatarajia kuwa na uwezo wa kujitegemea kwa asilimia hamsini kwa kipindi kifupi kijacho, ambapo kwa sasa ina uwezo wa kujitegemea kwa asilimia 42. 

Alisema hayo wakati wa mkutano maalum wa Baraza la Madiwani kupitia taarifa ya ufungaji hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2020/2021 uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa chuo cha Mipango Jijini Dodoma.

Mstahiki Meya Prof. Mwamfupe alisema kuwa juhudi za Mkurugenzi na Madiwani zimesaidia mapato ya halmashauri kuongezeka na kuifanya halmashauri kuwa na uwezo wa kujitegema kwa asilimia 42 hadi kufikia mwezi Juni 2021.

“Hongera sana Mkurugenzi na timu yako mmeweza kukamilisha kwa wakati taarifa ya hesabu, na kinachofurahisha zaidi ni uwezo wa kujitegemea, kama tumeweza kujitegemea kwa asilimia 42 tumebakiza asilimia 8 tungeweza kujitegemea kwa muda wa miezi sita, tulianza na asilimia 34 lakini sasa hivi tunakwenda vizuri, hongereni sana madiwani kwa matumizi mazuri na ukusanyaji mzuri wa mapato” alisema Prof. Mwamfupe.

Awali akiwasilisha taarifa hiyo ya hesabu mbele ya wajumbe wa baraza hilo, Mkuu wa Idara ya Fedha na Biashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA Rahab Philip alisema kuwa, uwezo wa kujitegemea umeongezeka kutoka asilimia 34 mwaka juzi hadi asilimia 42 mwaka jana hali inayoonesha kuwa tunapiga hatua.

“Mheshimiwa mwenyekiti, uwezo wa kulipa madeni unapimwa kwa kulinganisha mali za muda mfupi yaani ndani ya mwaka mmoja na madeni yanayotakiwa kulipwa ndani ya mwaka huo. Kwa mujibu wa kanuni na taratibu za fedha, uwiano wa 2:1 yaani thamani ya mali za muda mfupi inatakiwa kuwa mara mbili ya madeni ya muda mfupi. Uwezo wakulipa madeni kwa 2020/2021 umepungua kutoka uwiano wa 3.1:1 ya mwaka uliopita hadi 1.5:1 mwaka huu" alisema CPA Rahabu.

Kikao hicho kilichoongozwa na Mwenyekiti wake Prof. Mwamfupe, kilihudhuriwa na Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru ambaye ndiye Katibu, wajumbe ambao ni madiwani, wakuu wa idara pamoja na wageni mbalimbali.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru akiongea wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani uliohusu Taarifa ya Ufungaji Hesabu za Halmashauri ya Dodoma kwa Mwaka wa Fedha 2020/2021

Mkuu wa Idara ya Fedha na Biashara wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, CPA Rahab Philip alipokuwa akijibu hoja na kutolea ufafanuzi vipengele vya taarifa iliyowasilisha mbele ya Baraza la Madiwani.

Mjumbe wa Kamati ya Fedha na Utawala ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Zuzu, Mhe. Awadh Abdallah akichangia wakati wa Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa Jiji la Dodoma.

Diwani wa Kata ya Chang'ombe, Mhe. Bakari Fundikila alichangia hoja mara baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya Ufungaji wa Hesabu za Halmashauri kwa mwaka wa Fedha 2020/2021.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.