• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

"Haya ndio matunda ya Serikali inayowajali watu wake" - Waziri Jafo

Imewekwa tarehe: July 25th, 2019

SERIKALI imebatilisha uamuzi wa kuwaondoa wanafunzi 48 wa shule za vipaji maalumu ambao walipata daraja la tatu katika mtihani wa ndani wa muhula wa pili wa kidato cha sita kwenda shule za bweni za kawaida baada ya kupoteza nafasi ya kuendelea na masomo kwenye shule hizo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo alitoa kauli hiyo wakati alipokuwa kwenye ziara kwenye shule ya Sekondari ya Kilakala ya wasichana wenye vipaji maalumu iliyopo mkoani Morogoro.

“Leo (Julai 19, 2019) nitoe tangazo la wazi kwa wanafunzi wote 48, kuwa Serikali imefanya tathmini na imeona wanafunzi wote hao waendelee na masomo yao kwenye shule hizo kwa mpango maalumu… haya ndiyo matunda ya Serikali inayowajali watu wote,” alisema Jafo.

Alisema TAMISEMI kupitia wataalamu wake walitoa barua kwenda kwa Makatibu Tawala wa Mikoa ya Tanzania Bara ikiagiza juu ya uhamisho wa wanafunzi waliopata daraja la tatu hadi sifuri .

 “Siku za hivi karibuni wataalamu wangu walitoa maelekezo kwenye shule za vipaji maalumu kwa waliopata daraja la tatu hadi ziro wanatakiwa wahamishwe kwenda shule za serikali za bweni za kawaida na kubakia waliopata daraja la kwanza na la pili,” alisema Waziri Jafo.

Alisema serikali imetafakari na imeona wanafunzi hao 48 waliopaswa kuondolewa waendelee kubaki kwenye shule hizo.

Hata hivyo alisema wanafunzi hao wametakiwa waongeze juhudi kubwa za kusoma na wakuu wa shule hizo pamoja walimu wao kuandaa mpango mkakati wa kuwawezesha kufanya vyema katika masomo yao.

Waziri Jafo alisema hayo ni maelekezo maalumu ya serikali na kwamba wanafunzi hao na wengine hawatakiwi kubweteka ila wanapaswa kujitambua kuwa kuchaguliwa kwenye shule za vipaji maalumu haikuwa ni kwa bahati mbaya isipokuwa ufauli wao ni wa kiwango cha juu na unapaswa kuendelezwa wanapokuwa kwenye shule hizo.

“Wanafunzi hawa wajiwekeee utaratibu wa kusoma kwa juhudi kubwa na walimu wa masomo yao waandae vipindi vitakavyowawezesha kufanya vyema sawa na wengine kupata alama za juu,” alisisitiza Mhe. Jafo.

Alisema lengo la serikali ni kuona matokeo ya mtihani mwaka 2020 shule zake zisizopungua sita zinaingia kumi bora na hilo litawezekana iwapo wanafunzi watazingatia masomo pamoja na wakuu wa shule kuweka programu maalumu zitakazosimamiwa na walimu ili kuwezesha ufaulu wa daraja la kwanza.

Jafo alisema shule za sekondari za kata hasa zenye kidato cha sita zina kuja kwa kasi kubwa na kati ya Shule 100 bora, shule 52 kati ya 64 za serikiali ni za Kata jambo ambalo linazitishia Shule 12 za vipaji maalumu.

Chanzo: HabariLeo Online


Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.