• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hazina SACCOS yapongezwa kwa kushuka riba ya mikopo

Imewekwa tarehe: November 21st, 2020

CHAMA cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina SACCOS) kimepunguza riba ya mikopo kutoka asilimia 15 hadi 13 kwa mwaka sawa na wastani wa asilimia 1.5 kutoka asilimia 2 kwa mwezi ili kuwawezesha wanachama wake kupata mikopo kwa gharama nafuu.

Akifungua Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Hazina Saccos Jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. Doto James, ambaye hotuba yake ilisomwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Rasilimali Watu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Gisela Mugumira aliyemwakilisha, alisema kuwa hatua hiyo italeta manufaa kwa wanachama wake.

 “Nimefurahishwa na jambo hili la kushusha riba kwani ni mpango mkubwa wa Serikali kuona riba zinazotozwa na taasisi za fedha zinashuka zaidi ili kuinua maisha ya Watanzania, hivyo nawaelekeza muendelee kuona namna mnavyoweza kupunguza zaidi riba”, alisema Bi. Gisela.

Aidha, aliwataka viongozi na Bodi mpya itakayochaguliwa hapo kesho kuona ni namna gani itawawezesha wafanyakazi wote kufahamu na kujiunga na Hazina SACCOS, huku wakiongeza ubunifu wa bidhaa na huduma zinazolenga kutatua changamoto za wanachama na Watanzania kwa gharama nafuu.

Akizungumza kuhusu mpango wa Hazina SACCOS kuanza kuwalipia mikopo wanachama wanaodaiwa na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Bi. Gisela, alipongeza hatua hiyo akieleza kuwa itasaidia wanafunzi wengi kupata mikopo kwani itaboresha ukwasi wa Bodi hiyo.

“Ubunifu huu ni vema ukatambuliwa, maana naona umelenga zaidi kuwasaidia wanachama wenu kulipa mikopo hiyo kwa mkupuo na wakati huo huo kutunisha mfuko wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu.”Alieleza Bi Gisela.

Bi. Gisela, aliwaasa wajumbe wa mkutano kuwajibika na kuona kwamba Hazina SACCOS inasonga mbele na kukidhi mahitaji ya wanachama wake, huku ikiwa ya mfano kitaifa kwa sababu ndiyo SACCOS pekee nchini inayohudumia watumishi wote wa umma.

Aidha, alitoa rai kwa viongozi na wanachama kuongeza michango yao kila mwezi ili kuimarisha mfuko na kutoa elimu kwa wanachama juu ya umuhimu wa kujiwekea akiba.

Awali akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Bodi wa Hazina SACCOS anayemaliza muda wake Bw. Aliko Mwaiteleke alisema kuwa chama kimeendelea kutoa mikopo kwa wanachama wake ambapo mpaka kufikia tarehe 30 Septemba, 2020, jumla ya mikopo yenye thamani ya Sh. bilioni 4.33 imetolewa kwa Wanachama 951 kutoka taasisi mbalimbali za Serikali.

“Mikopo iliyotolewa mwaka huu ni sawa na ongezeko la asilimia 43 ambapo pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha ukopaji tumelipa maombi ya mikopo yote kwa wakati kwa kuzingatia taratibu za Chama,” Alisema Bwana Mwaiteleke.

Bwana Mwaiteleke, alisisitiza umuhimu wa wanachama kurejesha mikopo kwa wakati kwani ni miongoni mwa mambo yatakayosaidia kupungua zaidi kwa riba ya mikopo kama wengi wanavyotamani.

“Bodi inatarajia kufanya mapitio ya riba na gharama za maombi ya mkopo ili iwe asilimia 13 kwa mwaka, mikopo ya dharura na 'standing order' iwe kati ya asilimia 0.5 na 1.5 kwa mwezi”, Alisema Bw. Mwaiteleke.

Aliongeza kuwa kwa kipindi cha miezi tisa chama kimekusanya fedha kiasi cha Sh. bilioni 5 ikilinganishwa na kiasi cha Sh. bilioni 3.8 kilichokusanywa kwa kipindi kama hicho mwaka 2019.

Kwa upande wa uwekezaji Bw. Mwaiteleke alieleza kuwa uwekezaji kwenye mradi wa eneo la Njedengwa unaohusisha ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya kibiashara yakiwemo maduka makubwa, zoezi la kutafuta wawekezaji bado linaendelea na kamati ya uratibu wa mradi huo inaendelea na kazi hiyo.

Vile vile, katika kuboresha huduma za Chama, Chama kinaendelea zoezi la kujenga Mfumo wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano – TEHAMA utakao julikana kama Hazina SACCOS App, utakaowawezesha wanachama kupata taarifa zao kwa njia ya mtandao.

Hazina SACCOS ina wanachama takribani 5,000 ambao ni watumishi wa umma. Chama hicho kiko katika mkutano wa saba wa mwaka ambao unakutanisha wajumbe wa Mkutano Mkuu ili kupitia taarifa ya utendaji na maendeleo ya chama kwa kipindi cha miezi tisa kwa Mwaka 2020.

Meneja wa Hazina Saccos, Bw. Festo Mwaipaja, wakati wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Chama cha Ushirika wa Akiba na Mikopo cha Hazina (Hazina Saccos) katika Ukumbi wa Mikutano wa Karimjee Jijini Dar es Salaam.

Mwakilishi wa Mgeni rasmi, Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala na Rasilimali watu, Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Gisela Mugumira (walioketi-Katikati), akiwa pamoja na wajumbe wa Bodi ya Hazina SACCOS pamoja na Sekretarieti ya Chama hicho, wakati wa Mkutano Mkuu wa Saba wa Chama hicho unaofanyika Ukumbi wa Karimjee, Jijini Dar es Salaam.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.