• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera Hombolo Makulu ushirikishaji wananchi - CCM

Imewekwa tarehe: July 5th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Dodoma imefurahia juhudi za uongozi wa Kata ya Hombolo Makulu kuhamasisha wananchi kushiriki katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu iliyofikia asilimia 90.

Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM, Dkt. Damas Mkassa (pichani juu) alipoongoza Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua ujenzi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu iliyopo jijini Dodoma.

Dkt. Mkassa alisema “niwapongeze viongozi wa Kata ya Hombolo Makulu akiwemo Mheshimiwa Diwani wetu na Afisa Mtendaji wa Kata. Lakini pia wananchi na viongozi wa eneo hili kwa kutoa ushirikiano sababu nimesikia hapa kuna nguvu ya wananchi. Bila wananchi kuhimizwa kutoa nguvu zao hapa tusingefikia hii hatua ambayo tumefikia. Kwa hali halisi, mradi huu nafikiri umevuka asilimia 90, kwa maana hiyo tunatarajia mwakani mapema sana wanafunzi watakaofaulu wataweza kutumia shule hii”.

Mwenyekiti huyo alimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa fedha anazotoa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi. “Mkoa wa Dodoma ni mkoa wa mfano, katuletea miradi mingi na mingine tutaiona baadae. Lakini huu ni mfano mzuri wa kuigwa taarifa inaonesha wanafunzi walikuwa wanatembea zaidi ya kilometa tisa kufuata elimu. Kwa maana hiyo, tutakuwa tumewakomboa watoto wetu na hasa wa kike ambao wanakuwa kwenye maeneo hatarishi kwa kwenda kutafuta elimu mbali. Lakini pongezi za pili nizitoe kwa uongozi wa Wilaya ya Dodoma, Jiji la Dodoma Mkurugenzi wetu, Joseph Mafuru na timu yake ya wataalam kwa kusimamia vizuri ujenzi wa mradi huu” alisema Dkt. Mkassa.

Aidha, alishauri TARURA kuchonga barabara inayoelekea shuleni hapo ili irahisishe kusafirisha vifaa na wakaguzi kwenda kukagua shule hiyo.

Vilevile, alishauri kuchimbwa kisima katika shule hiyo ili kuwa na maji ya uhakika na kuepuka kunyang’anyana maji na wananchi.

“Suala la tatu ni umeme, nimeambiwa umeme hapa haujafika. TANESCO ni yetu na ipo mkoani kwetu, tutawaomba wakamilishe miundombinu ya umeme. Umeme utaimarisha usalama hapa, na maabara tatu tulizoziona hapa zitategemea umeme kufanya kazi, masomo ya kompyuta pia yatategemea umeme kufanya kazi. Kwa ujumla sisi Kamati ya Siasa ya Mkoa, mimi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa tumeuona mradi na tumeupokea vizuri. Mradi ni mzuri unatia moyo na tunatoa pongezi kwa Mwenyekiti wetu wa CCM na Rais wa Jamhuri wa Jamhuri kwa kazi kubwa ambayo ameifanya kwa Dodoma” alisema Dkt. Mkassa.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu, mkuu wa shule hiyo, Joseph Kavarambi alisema kuwa ujenzi ulianza tarehe 25 Januari, 2022 kwa ufadhili wa mradi wa kuboresha elimu ya sekondari “SEQUIP” kwa gharama ya shilingi 600,000,000 mpaka utakapokamilika. Alisema kuwa katika awamu ya kwanza shilingi 470,000,000 zilitolewa.

Kavarambi alisema kuwa ujenzi huo unatumia utaratibu wa force account, awamu ya kwanza imehusisha ujenzi wa vyumba vinane vya madarasa, jengo la utawala, maabara tatu za sayansi, jengo la ‘ICT’, maktaba na matundu 20 ya vyoo.

Alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo utawasaidia wanafunzi kuwa na mazingira bora ya kujifunzia na kufundishia. Mradi umetoa ajira kwa wananchi wanaoishi maeneo ya jirani kwa kushiriki katika kazi za ujenzi na uuzaji vyakula.

Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri aliishukuru kamati hiyo kwa kutembelea mradi huo. “Mheshimiwa mwenyekiti mimi nakushukuru sana kufika eneo hili la Hombolo Makulu na kufanya ukaguzi, lakini pia kutoa tathmini ya ukaguzi wako kwa namna ya kisomi sana, katika masuala ya msingi sana ambayo umeyasema. Kwa niaba ya wenzangu wote kwenye msafara huu tunakushukuru sana kwa maoni na maelekezo ambayo umeyatoa na tunakupongeza kwa kufanya kazi kwa weledi.

“Lakini ni sahihi kabisa na sisi tunaungana na viongozi wa chama mkoa kutoa pongezi za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kwa kututengea fedha na kutupatia shilingi 600,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ya Hombolo Makulu. Taarifa unayo, lakini tukili tulipokea shilingi 470,000,000 za awali na zikafanya kazi kwa kiwango hiki unachokiona. Ujenzi wa madarasa nane ambayo yanakiwango kizuri sana, ujenzi wa maktaba, shule hii itakuwa na maktaba ya kisasa sana. Ujenzi wa chumba cha kompyuta na ujenzi wa maabara tatu pamoja na maeneo ya maliwato kwa wanafunzi wetu na wenye mahitaji maalum pamoja na chumba cha kubadilishia” alisema Shekimweri.

Alisema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa maono mapana ya Rais. “Zaidi ya kutupatia shilingi bilioni 2.86 kwa Jiji la Dodoma ya kujenga madarasa ya UVIKO-19, bado katupatia shilingi 600,000,000 ya kujenga hii shule ya Hombolo Makulu. Mheshimiwa Rais katika wilaya yetu hii, Jiji kaliweka kwenye moyo wake na sisi tunaemsaidia majukumu katika maeneo haya tumhakikishie tutaendelea kusimamia fedha hizi vizuri na muda wote tupo ‘site’ kusimamia fedha hizi” alisisitiza Shekimweri.

Akiongelea changamoto za maji, barabara na umeme, alisema kuwa wilaya yake inazifahamu. “Nikuhakikishie tunazifahamu na wadau wote wapo hata. Nguzo zimeshaanza kuja hapa. Ni jambo la muda, tuna muda mrefu hadi kufikia Desemba, maandalizi ya kuwapokea wanafunzi hapa shuleni. Tumeshatoa maelekezo ya kuanza taratibu za usajili wa shule hii” alisema Shekimweri.

Nae mzazi Agatha Kihori alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo ni mkombozi kwa wanafunzi wa Kata ya Hombolo Makulu. “Wanafunzi walikuwa wanatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Kuna wakati mzazi unafikiria mtoto atarudi kweli salama. Tunaishukuru sana serikali kwa ujenzi wa shule hii” alisema Kihori.

Ukamilishaji wa shule ya sekondari Hombolo Makulu utaifanya Kata ya Hombolo Makulu kuwa na shule yake ya kwanza ya sekondari.

Wajumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Dodoma walipotembelea na kukagua ujenzi wa shule ya sekondari Hombolo Makulu iliyopo jijini Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.