• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera Jiji, Halmashauri zote Dodoma fatilieni miti inayopandwa - Dkt. Mahenge

Imewekwa tarehe: January 23rd, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma Dkt. Binilith Mahenge amempongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa mikakati ya upandaji miti baada ya kugawanya Wakuu wa Idara wa Halmashauri hiyo katika Mitaa mbalimbali kusimamia zoezi la upandaji miti jambo ambalo litaongeza kasi ya zoezi hilo Jijini hapa.

Dkt. Mahenge ameyasema hayo leo alipoongoza zoezi la upandaji miti katika Kata ya Mkonze Mtaa wa Miganga ambapo zaidi ya miti 2000 imepandwa katika eneo hilo.

Aidha, Dkt Binilith Mahenge amewataka viongozi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Dodoma kujenga utaratibu wa kutembelea na kufuatilia maeneo yote yanayopandwa miti kuona maendeleo ya miti hiyo kama inahudumiwa ili kuona matokeo mazuri ya zoezi hilo.

Dkt Mahenge amesema zoezi hilo ambalo mwitikio wake umekuwa mzuri lakini kama ufuatiliaji hautafanywa hakutakuwa na matokeo yaliyotarajiwa.

“Zoezi hili ni zuri sana lakini kama hatufanyi ufuatiliaji zoezi hili halina maana, hakikisheni mnafuatilia maeneo yote yaliyopandwa miti ili kuona namna inavyoendelea” amesema Dkt Mahenge.

Vile vile, amewapongeza Wananchi wa Mtaa wa Miganga kwa kujitokeza kwa wingi katika zoezi hilo na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri, Meneja TARURA na TANESCO kuhakikisha wanatoa kipaumbele kupeleka huduma zote muhimu katika eneo hilo huku akisema kuwa hayo ndio matunda na faida za kuwa wazalendo na kujitokeza kufanya mambo ya kijamii.

“Nataka mtaa huu upewe kipaumbele na ninaanza na eneo hili tulipo hii ilikua barabara kubwa ya Mkoa lakini imetelekezwa hivi, hivyo natoa siku tano kwa TARURA kuhakikisha barabara hii inapitika, lakini pia huduma ya umeme na upimwaji wa viwanja uzingatie sana mtaa huu kwa sababu wamejitokeza kwa wingi kuunga mkono juhudi za Serikali za kukijanisha Dodoma.” Alisema Dkt. Mahenge.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma Joseph Mafuru amesema kuwa leo wameonesha aina nyingine ya upandaji wa miti kwa kupanda pembezoni mwa barabara tofauti na ilivyozoeleka katika Jumamosi zilizopita lengo ni kuufanya mji uwe katika mandhari nzuri na kuweka vivuli katika barabara za Jiji hilo.

Mafuru ameongeza kuwa jumamosi ijayo ni ya usafi lakini hilo haliwazuii wao kuendelea kupanda miti kwani zoezi hilo pia ni miongoni mwa njia mojawapo ya kutunza mazingira.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Bilinilith Mahenge akiongea na wananchi waliojitokeza kwenye zoezi la kupanda miti Mtaa wa Miganga Jijini Dodoma. Dkt. Mahenge aliongoza zoezi hilo ambao lilifanyika asubuhi ya leo.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma Joseph Mafuru akiongea kuhusu mikakati ambayo Halmashauri imejiwekea ili kuhakikisha zoezi la kukijanisha Dodoma linafanikiwa.


Mkuu wa Idara ya Usafi wa Mazingira na udhibiti wa taka ngumu wa Jiji Dickson Kimaro akifafanua jinsi Jiji lilivyojipanga pamoja na TFS kuhakikisha miche ya miti inapatikana kwa ajili ya kulifanikisha zoezi la kukijanisha Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.