• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera Rais Samia, barabara ya lami Nzuguni

Imewekwa tarehe: July 5th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa uongozi bora na kutoa fedha shilingi 6,109,748,702.50 za tozo ya Mafuta kujenga barabara ya Nzuguni - Mahomanyika kilometa 5.0 kwa kiwango cha lami.

Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Damas Mkassa alipoongoza Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa wa Dodoma kutembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Nzuguni Mahomanyika inayojengwa kwa kiwango cha lami.

Dkt. Mkassa alisema “nitangulize shukrani na pongezi kwa Rais, Samia Suluhu Hassan kwa uongozi bora na kazi nzuri. Fedha hizi nasikia zimetokana na tozo ya mafuta na kuna watu walikuwa wanapiga kelele juu ya tozo ila tunaona matokeo makubwa ya hizo tozo. Na siku zote mkuu wa nchi anapotoa maelekezo anakuwa ameona mbali. Tunaweza tusione matokeo mwanzo ila tunaweza kuona sasa hizi kilometa za barabara zinakwenda kujengwa hapa. Barabara hii ina umuhimu mkubwa sababu inatuunganisha na vitu vikubwa. Inatuunganisha na barabara kuu ya Dar es Salaam, inatuunganisha na Soko kuu la Job Ndugai, kutuo kikuu cha mabasi Dodoma hadi ‘ring road’ na hadi nyumba 350, ni muhimu sana kwa barabara hizi zinapokuwa katika jiji”.

Akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Nzuguni Mahomanyika (kilometa 5.0) kwa kiwango cha lami, Mhandisi wa TARURA, Revocatus Nsubile alisema kuwa mradi huo upo chini ya Mkandarasi Nyanza Road Works co Ltd.

Alisema kuwa mradi huo unatekelezwa kwa gharama ya shilingi 6,109,748,702.50. “Mkataba una miezi 12 na ulianza tarehe 5.4.2022 na unatarajiwa kukamilika tarehe 5.4.2023. Mradi una asilimia 28 zaidi ya asilimia 23 kiwango mradi uliotakiwa kuwa sasa. Hadi sasa hakuna mabadiliko ya gharama ya mradi na hatutarajii kuyapata” alisema Mhandisi Nsubile. 

Akitoa ufafanuzi wa mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma, Jabir Shekimweri alisema kuwa barabara hiyo ni ya kimkakati. “Mradi huu ulikuwa chini ya TARURA kwa ujenzi wa kilometa 1.55 lakini kwenye ziara ya Waziri wa Nchi- TAMISEMI, tuliweza kumpatia taarifa na nichukue nafasi hii kumpongeza Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde ambaye aliwasilisha ombi kwa serikali kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii kimkakati. Barabara hii inaunganisha mashamba ya mjini ‘urban farms’ ya Hombolo pamoja na Vikonje lakini inaunganisha makazi mapya yanayojengwa na TBA nyumba 350, lakini pia inatuunganisha na uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Msalato ambao upo kwenye ujenzi. Babaraba hii inaunganisha na barabara ya Pete ya mzunguko, ni barabara inayotuunganisha na Soko Kuu la Job Ndugai, Kituo Kikuu cha Mabasi ya mikoani, lakini pia uwanja wa maonesho wa Nanenane lakini pia uwanja wa mpira utakaojengwa Nzuguni” alisema Shekimweri.

Mkuu wa wilaya aliitaja barabara hiyo kuwa ya kipekee. “Baada ya hoja hiyo, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan alitoa maelekezo kwa TAMISEMI na waziri aliyatamka hapa kwamba tutaogezewe kilometa tano na hivyo, kujenga kwa kiwango cha lami nusu ya barabara hii kilometa 13. Ni matarajio yetu barabara hii ikikamilika kilometa 6.5 kwa bajeti inayokuja itaendelea kuwa kipaombele ili iweze kufikia matarajio ambayo kila mtu anayo” alisema Shekimweri.

Aidha, alimpongeza Diwani wa Kata ya Nzuguni kwa kazi nzuri na kutoa ushirikiano mkubwa kwenye kuwaelimisha wananchi kulinda mradi huo.

Jeremiah Chongo ambae ni mkazi wa Mahomanyika alisema kuwa barabara hicho itachangia kukuza uchumi wa maeneo mbalimbali ya jiji hilo. Alisema kuwa ujenzi wa barabara kama ulivyo ujenzi wa miundombinu mingine ni kichocheo cha maendeleo ya maeneo mbalimbali kwa sababu inafungua fursa za kibiashara.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.