• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera Rais Samia kuimarisha miundombinu, maslahi ya watumishi - CD Mafuru

Imewekwa tarehe: May 30th, 2022

Na. Dennis Gondwe, DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kuimarisha miundombinu na maslahi ya watumishi katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma jambo lililoamsha ari ya kazi kwa watumishi hao.

Pongezi hizo zilitolewa na Mwenyekiti wa Wakurugenzi wa Halmashauri za Mkoa wa Dodoma katika tukio hilo, Joseph Mafuru alipotoa neno kwa niaba ya Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa za Mkoa wa Dodoma katika ukumbi wa mikutano wa PSSSF leo katika hafla ya kumshukuru na kumpongeza Rais kwa kuboresha maslahi ya watumishi.

Mkurugenzi Mafuru alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anaimarisha miundombinu kwa kasi kubwa. “Mimi kama mkuu wa taasisi wa Jiji la Dodoma ninaona sura na kazi ya utendaji ilivyobadilika mapema baada ya kusikia matangazo ya nyongeza ya mshahara. Watumishi unawaona wanafanya kazi kwa kasi. Ukienda kwenye kata unawakuta, ukienda kwenye mitaa unawakuta wanasimamia miradi ya maendeleo kwa kasi kubwa. Hii inatasfiri kubwa sana kwamba morali imerudi juu. Maana yake tutegemee matokeo kubwa kwenye huduma za wananchi na huduma za jamii kwa ujumla” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Alisema kuwa kuanzia mwezi Julai mambo mengi yanakwenda kubadilika baada ya mishahara kubadilika. “Tuna madeni mawili, moja kasi ya utoaji wa huduma za uhakika lazima tuoneshe nini kimebadilika kwetu, isije fika mwezi Agosti au Septemba, wananchi wanaona huduma ni ileile kama ambavyo ilikuwa miaka miwili ya nyuma” alisema Mafuru.

Mwenyekiti huyo wa Wakurugenzi wa Mkoa wa Dodoma alisema kuwa Rais ameendelea kuboresha miundombinu kwa ujenzi wa barabara ya mzunguko “ring road” inayozunguka Jiji la Dodoma. “Tafsiri yake ni kwenda kufungua uchumi pembezoni mwa Jiji la Dodoma. Maana yake nyongeza ya mishahara ipo, kuna watu wana “arreas” mpaka milioni 40 na milioni 20 katika akaunti zao. Maana yake twende tukafanye uwekezaji. Twende tukajenge viwanda, hoteli na vituo vya Mafuta kwa ajili ya faida yetu na pili kwa ajili ya kuzalisha ajira” alisema Mkurugenzi Mafuru.

Awali Katibu Tawala Mkoa wa Dodoma, Dkt. Fatuma Mganga alisema kuwa hafla hiyo ililenga kumpongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa nyongeza ya mishahara na posho za wafanyakazi. “Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa ulielekeza kuwa leo tukutane watumishi wote ambao tumepata bahati ya kupata ajira serikalini, tunakutana hapa kwa jukumu kuu moja, sisi sote ni watanzania tumepata ajira ya kuwatumikia watanzania wenzetu. Lakini imepita miaka mingi tokea watumishi hawa waweze kupata nyongeza katika mishahara yao. Lakini kama haitoshi, posho za kufanya kazi mbalimbali, posho za safari zimekuwa katika kiwango hicho ambacho tunacho kwa muda mrefu sana kwa kupitia mawazo ya Mkuu wa Mkoa akasema ni busara tukutanike hapa kwa ajili ya kumpoongeza na kumshukuru Rais Samia kwa hiki alichokifanya kwa wananchi wote” alisema Dkt. Mganga.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.