• Wasiliana nasi |
    • Maswali na majibu |
    • Baruapepe - Watumishi |
    • eVibali |
    • Malalamiko |
Dodoma City Council
Dodoma City Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Jiji la Dodoma

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii, Ustawi wa Jamii, Jinsia na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Udhibiti wa Taka ngumu
    • Vitengo
      • Sheria na Usalama
      • Mkaguzi wa Ndani
      • TEHAMA na Uhusiano
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuji
    • Ward
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Mji wa Serikali
    • Kwa nini uwekeze Dodoma?
  • Huduma Zetu
    • Maendeleo ya jamii
    • Elimu
    • Miundombinu
    • Mazingira
    • Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Utawala
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Kudhitibi UKIMWI
      • Maadili
    • Kamati zingine/Bodi/Uwakilishi
    • Ratiba
      • Vikao vya Madiwani
      • Kuonana na Mstahiki Meya
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Ripoti
    • Sheria Ndogo
    • Miongozo
    • Mpango Mkakati
    • Fomu
    • Jifunze Nyumbani
    • Mpango Kabambe
    • Jarida
    • Asemavyo Mahia - Afya na Mazingira
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
    • Habari
    • Matukio
  • City TV

Hongera watumishi wa Jiji kwa kupanda miti - Dkt. Mahenge

Imewekwa tarehe: January 16th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Dkt. Binilith Mahenge ameridhishwa na mwanzo wa utekelezaji wa agizo lake kwa watumishi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma la kupanda miti katika maeneo mbalimbali ya jiji hilo.

Dkt. Mahenge alionesha kuridhishwa alipokuwa akitoa salamu za shukrani baada ya kukamilika kwa zoezi la upandaji miti lililochukua masaa matatu katika eneo la Iseni Park jijini hapa.

“Napenda kuwapongeza na kuwashukuru sana kwa mwitikio wenu katika zoezi hili la upandaji miti. Wingi huu umelifanya zoezi la upandaji miti kuwa jepesi na kitendo cha furaha kwetu sote. Leo tumepanda miti zaidi ya 3,700 kutokana na umoja tulionao. Tukiwa na nguvu hii kwa kata zote Dodoma ya kijani tunaifikia mapema zaidi. Hivyo, nimeona ni jambo la uungwana watu wakifanya kazi nzuri kupewa shukrani” alisema Dkt. Mahenge.

Aidha, alipongeza mkakati wa halmashauri hiyo wa kuzishirikisha ofisi za kata kwenye zoezi la upandaji miti katika maeneo yao. “Ni vizuri halmashauri ikasimamia utekelezaji na tujitahidi kila mtu amuombe Mungu kwamba apate nguvu ya kuwajibika kuitunza sayari yetu ili tupate vile ambavyo tunavihitaji katika sayari hii. Miti hii tunayopanda inaenda kuvuna hewa ukaa. Dodoma ya kijani itawezekana kama nguvu yetu hii iliyojitokeza leo kuja kupanda miti itaendelea kujitokeza na kushiriki katika mazoezi ya kupanda miti. Ndiyo maana tukaona sisi kama viongozi lazima tuoneshe njia kwa kujitokeza mara kwa mara katika mazoezi ya upandaji miti ili kutoa hamasa kwa jamii” alisema Dkt. Mahenge.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru alisema kuwa zoezi hilo ni muendelezo wa kazi iliyoanza wiki iliyopita ya kupanda miti. “Hili eneo Iseni park zamani ndilo lilipangwa kuwa makao makuu, yaani mji wa serikali mtumba ‘National Capital Center’ kwa mujibu wa Mpango Kabambe wa mwaka 1976. Maamuzi ya sasa, eneo hili zijengwe ofisi za wizara na zitakazo baki zitapelekwa eneo la Kizota ambazo ni kubwa kama eneo hili” alisema Mafuru.

Wakati huohuo, Mkuu wa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu katika Jiji la Dodoma, Dickson Kimaro alisema kuwa zoezi la upandaji miti ni endelevu kwa lengo la kukijanisha Dodoma. “Eneo hili lina ekari 37, ni eneo la wazi. Leo kuna mashimo 3,700 na miti iliyokuja hapa ni 4,000. Tukumbuke kuwa katika mji mikubwa kuna misitu ya mjini kwa lengo la kuusaidia mji kupumua na kuondoa uharibifu wa mazingira kwa njia ya hewa” alisema Kimaro.

Joseph Fungo, ambae ni Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA na Uhusiano katika Jiji la Dodoma alisema kuwa zoezi hilo ni zuri kwa mustakabali wa Jiji hilo. “Kama unavyofahamu ni wajibu wa Halmashauri ya Jiji la Dodoma kutoa huduma kwa wananchi na kupendezesha Jiji la Dodoma. Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa alitoa agizo kwa watumishi wote kushiriki katika zoezi la upandaji miti. Kitengo chetu kama sehemu ya halmashauri tulihakikisha watumishi wote na wananchi wanapata taarifa ya zoezi hili ili wafike eneo hili kwa ajili ya kupanda miti. Matangazo ya barabarani, tovuti, mbao za matangazo na mitandao ya kijamii ili kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa” alisema Fungo. Zoezi hilo siyo la watumishi wa jiji pekee, ni jukumu la jamii nzima, aliongeza.

Ikumbukwe kuwa tarehe 9 Januari, 2021 mkuu wa mkoa wa Dodoma alipokuwa akizindua zoezi la upandaji miti katika utekelezaji wa kampeni ya kijanisha Dodoma aliagiza kila mtumishi wa Jiji la Dodoma kupanda miti 10 kila wiki katika majira ya mvua.

Afisa Habari wa timu ya Dodoma Jiji FC, Moses mpunga akipanda mti eneo la Iseni Park Jijini Dodoma.


Mchumi Jiji la Dodoma, Shaban Juma akipanda mti eneo la Iseni Park Jijini Dodoma.

Matangazo

  • MKUTANO WA BARAZA LA WAHESHIMIWA MADIWANI January 30, 2025
  • KITUO CHA AFYA ILAZO KIMEANZA KUTOA HUDUMA January 13, 2025
  • HOSPITALI YA JIJI LA DODOMA IMEANZA KUTOA HUDUMA ZA AFYA January 12, 2025
  • TANGAZO LA UUZWAJI WA VIWANJA KIKOMBO December 03, 2024
  • Angalia zote

Habari za hivi punde

  • Barabara ya Lami ya Kilometa 6 yawanufaisha wakazi wa Kata ya Miyuji

    April 23, 2025
  • Huduma ya Chakula na Lishe yapandisha ufaulu Shule ya Sekondari Nala

    April 22, 2025
  • Mradi wa Maji Nala wa Bil. 1.3, mkombozi kwa wananchi

    April 22, 2025
  • Milioni 500 kukamilisha mradi wa Kituo cha Afya Kizota

    April 22, 2025
  • Angalia zote

Video

Watendaji Kata Wilaya ya Dodoma watakiwa kusimamia maswala ya Lishe
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Historia ya Manispaa
  • Wasifu wa Manispaa
  • Kata na Madiwani
  • Mji wa Serikali
  • Orodha ya Madiwani
  • Mpango Mkakati wa Halmashauri (SP)
  • Kwanini uwekeze Dodoma?
  • Zabuni za Wakala wa Ukusanyaji Mapato
  • Zabuni ya Usafi wa Mazingira

Viunganishi Linganifu

  • Msalato Sekondari
  • Mkoa wa Dodoma
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • Chuo Kikuu Dodoma (UDOM)
  • Bunge

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani elekezi

Wasiliana nasi

    1 CDA Street, 40477

    Anuani ya posta: 1249, DODOMA, TANZANIA

    Simu: +255 26 232 4817

    Simu ya kiganjani:

    Baruapepe: cd@dodomacc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya tovuti

Copyright ©2017 The City Council of Dodoma. All rights reserved.